HIZI ndizo mpya za msimu ujao za Manchester United?
Jezi
mpya za Mashetani Wekundu zimevuja kwenye mitandao ya kijamii, ambazo
ni za Nike zikiwa na rangi nyekundu na chata la rangi nyeupe wadhamini
wapya, Chevrolet kwa mbele.
Jezi hizo zina zipu nyeusi kutokea shingoni kuelekea chini na ufito mweusi kwenye pindo za mikono na mabegani.
Pamoja
na hayo haijathibishwa kama habari kuhusu jezi hizo ni sahihi. United
ilitangaza Julai mwaka 2012 udhamini wa jezi na Chevrolet, ambao
watakuwa wakilipa Pauni Milioni 25 kwa mwaka kuweka jina lao kwenye jezi
za timu hiyo kuanzia msimu ujao.
Wadhamini wa sasa wa United, Aon, hawataonekana tena kwenye jezi za timu hiyo kuanzia msimu ujao.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England wanaweza kuvuna fedha zaidi kutokana na ongezeko la dau la udhamini wa vifaa vya michezo.


