Friday, 7 March 2014

JEZI MPYA ZA MAN UNITED ZA MSIMU UJAO HIZI HAPA ZIKIWA NA CHATA LA WADHAMINI WAPYA


Ni hizi kweli? Picha hii imevuja kutoka kwenye mitandao ya kijamii
HIZI ndizo mpya za msimu ujao za Manchester United?
Jezi mpya za Mashetani Wekundu zimevuja kwenye mitandao ya kijamii, ambazo ni za Nike zikiwa na rangi nyekundu na chata la rangi nyeupe wadhamini wapya, Chevrolet kwa mbele.
Jezi hizo zina zipu nyeusi kutokea shingoni kuelekea chini na ufito mweusi kwenye pindo za mikono na mabegani.
Pamoja na hayo haijathibishwa kama habari kuhusu jezi hizo ni sahihi. United ilitangaza Julai mwaka 2012 udhamini wa jezi na Chevrolet, ambao watakuwa wakilipa Pauni Milioni 25 kwa mwaka kuweka jina lao kwenye jezi za timu hiyo kuanzia msimu ujao. 
Wadhamini wa sasa wa United, Aon, hawataonekana tena kwenye jezi za timu hiyo kuanzia msimu ujao.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England wanaweza kuvuna fedha zaidi kutokana na ongezeko la dau la udhamini wa vifaa vya michezo. 

HEEE JAMANI HAYA MAZITO SASA..!!! JIONEE PICHA YA HUYU MWANAMKE ALIEOA WANAUME 2

MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, wilayani Katavi, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Thursday, 6 March 2014

BREAKING NEWS,,BUNGE LA KATIBA LA AIRISHWA ,SABABU IKO HAPA




bungeee
Kutoka Mjengoni Dodoma Bunge la kujadili katiba limehairishwa na Mwenyekiti baada ya kutokea kwa vurugu baada ya kutoelewana kwa baadhi  wabunge kati ya Mh. Aboubakary ambaye ni Mwanasheria mkuu wa serikali ya Zanzibar alipomuomba Mheshimiwa Mwenyekiti asikubali kuruhusu baadhi ya majina ya wachangiaji wakati majina hayo hayajafika kwenye kamati inayohusika na uratibu wa rasimu.

Wednesday, 5 March 2014

NEYMAR APIGA HATITRIKI BRAZIL IKIICHAKAZA BAFANABAFANA MAGOLI 5 KWA 0,,,MATOKEO MENGINE MECHI ZOTE ZA JANA.




>>TIMU ZAMUENZI MADIBA, ZAVAA 46664!!
BRAZIL, Wenyejji wa Fainali za Mwaka huu za Kombe la Dunia Mwezi Juni, Leo huko FNB Stadium, Johannesburg, wamewanyuka Wenyeji wao South Africa Bao 5-0 kwenye Mechi ya Kirafiki ambayo pia ilkuwa ya kumuenzi Kiongozi Marehemu Nelson Mandela ambapo Bafana Bafana walivaa Jezi zenye Namba 46665, Namba ya ‘Mfungwa’ Madiba alipokuwa Jela, na Brazil kuingia Kipindi cha Pili wakibadili Jezi zao za kawaida za Njano na kuvaa Bluu huku wakiwa na Utepe Mkononi wenye Namba 46664.

RONALDO APIGA MBILI URENO IKIIKUNG'UTA MKONO CAMEROON...SASA NDIYE MKALI WA MABAO MILELE URENO


>>TIMU ZAMUENZI MADIBA, ZAVAA 46664!!
BRAZIL, Wenyejji wa Fainali za Mwaka huu za Kombe la Dunia Mwezi Juni, Leo huko FNB Stadium, Johannesburg, wamewanyuka Wenyeji wao South Africa Bao 5-0 kwenye Mechi ya Kirafiki ambayo pia ilkuwa ya kumuenzi Kiongozi Marehemu Nelson Mandela ambapo Bafana Bafana walivaa Jezi zenye Namba 46665, Namba ya ‘Mfungwa’ Madiba alipokuwa Jela, na Brazil kuingia Kipindi cha Pili wakibadili Jezi zao za kawaida za Njano na kuvaa Bluu huku wakiwa na Utepe Mkononi wenye Namba 46664.

RONALDO APIGA MBILI URENO IKIIKUNG'UTA MKONO CAMEROON...SASA NDIYE MKALI WA MABAO MILELE URENO

MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo jana ameifungia mabao mawili Ureno ikiitandika 5-1 Cameroon katika mchezo wa kirafiki na kuwa mchezaji aliyeifungia mabao mengi zaidi Ureno kihistoria.
Ronaldo sasa amefikisha jumla ya 49 aliyoifungia Ureno, mawili zaidi ya Pauleta aliyekuwa anaongoza.

MESSI AUGUA GHAFLA UWANJANI ARGENTINA IKILAZIMISHWA SARE YA 0-0 NA ROMANIA

MSHAMBULIAJI Lionel Messi jana aliugua Uwanja wa Taifa wa Bucharest wakati Argentina ikilazimishwa sare ya bila kufungana na Romania.
Mshambuliaji huyo wa Barcelona alishindwa kuibomoa safu kali ya ulinzi ya Romania katika mchezo huo.
Messi aliuanza taratibu mchezo huo na ghafla akajiinamia uwanjani dakika ya saba muda mfupi baada ya kupiga mpira wa adhabu. 
Baada ya mechi, Messi akasema juu ya maradhi yake: "Hii ni hali ambayo wakati wote inanitokea, imetokea mara chache nikiwa na Barça. Si kitu kwangu,".


Anajisikia vibaya: Lionel Messi akiwa amejiinamia baada ya kujisikia vibaya wakati wa mchezo dhidi ya Romania jana