Sunday, 21 February 2016

Hii ndio list ya viwanja 10 vyenye thamani zaidi Afrika, Tanzania je?


Huenda ukawa upo Tanzania lakini hili ukawa hulifahamu mtu wangu, tumezoea kusikia kuwa Tanzania ni nchi ambayo inatambulishwa vivutio vya utalii hususani mlima Kilimanjaro.

Wednesday, 17 February 2016

Jionee hapa TOP 5 ya simu za gharama zaidi duniani kwa mwaka 2015/2016

Mtu wangu wa nguvu kama bado hujakutana na list ya zinazotajwa kuwa simu zenye thamani zaidi duniani, mtu wako wa nguvu nimekutana nayo list hiyo, mara nyingi tumezoea kuona na kusikia mtu akinunua simu kwa gharama ya juu huenda ikawa ni kati ya Tsh milioni 1 hadi milioni mbili, ila hii ni TOP 5 ya simu kali na zenye thama duniani

Monday, 8 February 2016

KWA MARA YA KWANZA JIJINI MWANZA LIMEFANYIKA SHINDANO LA (MISS ALBINO MWANZA) NA KUPATIKANA MSHINDI,...JIONEE PICHA HAPA ZAIDI YA 30.

Shindano la miss Albino limefanyika jijini mwanza ili kumpata mwakilishi ambaye atawaiwakilsha mwanza katika shindano la miss Albino Tanzania.

Washiriki wakiingia ukumbi wa Gold Crest   kwa ajili ya kuanza shindano.

Thursday, 4 February 2016

WABUNGE WA SIMBA SC WAMEJUMUIKA NA WACHEZAJI WA SIMBA WAKIWA NJIANI KUELEKEA SHINYANGA.


Simba imesimama kwa muda mjini Dodoma na kuzungumza na baadhi ya wabunge wakiwemo Azzan Zungu, Juma Nkamia na wengine wenye mapenzi na kikosi cha Mnyama.

Wednesday, 3 February 2016

GOLI LA VARDY LAMKUNA KLOPP, ATOBOA ALICHOTAKA KUFANYA



Vardy 3
Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp katika hali isiyokuwa ya kawaida ameibukia na kutoa kauli kuwa nusura ampigie  makofi mshambuliaji wa Leicester City Jamie Vardy kutokana na goli alilolifunga dhidi ya Liverpool janausiku.

Jionee hapa Mahali ilipo na muonekano wake wa sasa bastola ya dhahabu ya Muammar Gaddafi


Ni miaka minne imepita toka auwawe aliyekuwa Rais wa Libya kanali Muammar Gaddafi na vikundi vya waasi wa nchi hiyo, Gaddafi alikuwa kiongozi ambaye ana miliki vitu vya thamani kubwa kama gari la kifahari lakini alikuwa ana miliki Bastola iliyopambwa kwa dhahabu.

Monday, 25 January 2016

HATIMAYE KATUMBI AAFIKI SAMATTA KWENDA GENK, KIJANA ANATUA DAR KESHO KWA SAFARI YA UBELGIJI KWENDA KUANZA MAISHA MAPYA


HATIMAYE bilionea Moise Katumbi Chapwe, Rais wa klabu ya TP Mazembe ya DRC amekubali mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ajiunge na KRC Genk ya Ligi Kuu ya Ubelgiji. Na Samatta anatarajiwa kurejea Dar es Salaam kesho kwa ajili ya safari ya Ubelgiji kwenda kuanza maisha mapya katika soka ya Ulaya. Samatta tayari amekwishasaini Mkataba wa awali na Genk wa miaka minne na sasa anakwenda kukamilisha taratibu. Samatta na Genk wanataka kukimbizana na muda ili kuwahi kabla ya dirisha dogo la usajili  halijafungwa, angalau mapema Februari Mwanasoka huyo Bora Anayecheza Afrika aanze kucheza Ubelgiji.

 
 

Meneja wa Samatta, Jamal Kisongo amesema kwamba Katumbi ameridhia Samatta aende klabu anayopenda.