Thursday, 27 February 2014

WENGER AWAJIA JUU WANAOMPONDA,RVP AMTETEA MOYES.

PDF
>>VAN PERSIE: MPENI MOYES MUDA!
RVP_N_MOYESJIJINI London, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amegeuka mbogo kwa Watu waliomponda kwa kuwapa Ofu ya Siku 2 Wachezaji wake na huko Manchester, Nahodha wa zamani wa Arsenal, Robin van Persie, amemtetea Meneja wa Klabu yake Manchester United, David Moyes, licha ya kukiri walicheza ovyo Mechi na Olympiacos waliyotwangwa 2-0.

VAN PERSIE: MPENI MOYES MUDA!
Robin van Persie ameieleza Manchester United kama ni "mbovu" lakini amesisitiza David Moyes anahitaji muda ili kurekebisha mambo Old Trafford.
Msimu wa Man United ulizidi kudidimia Jumanne Usiku wakati walipofungwa 2-0 huko Ugiriki na Olympiacos katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Ukichukulia Man United, ambao ndio Mabingwa Watetezi, wapo Pointi 11 nyuma ya Timu ya 4 kwenye Ligi Kuu England na wapo Pointi 15 nyuma ya Vinara Chelsea, baadhi ya Watu wamedai Moyes yupo njiani kupigwa Buti.
Lakini Robin van Persie amemtetea Moyes kwa kusema: “Yeye ni mpya na anahitaji muda. Anafanya bidii pamoja na sisi. Ni rahisi kumyooshea kidole Meneja lakini ni sisi tunatakiwa kuleta mafanikio Uwanjani.”
Licha ya kukiri huu ni Msimu mbovu kwao, Robin van Persie amesisitiza kuwa upo uwezekano mkubwa wa kuwabwaga Olympiacos katika Mechi ya Marudiano Old Trafford hapo Machi 19.
ARSENE WENGER: AWASHAMBULIA WALIOMPONDA KUWAPA OFU WACHEZAJI!WENGER-PROFESA
Arsene Wenger amejibu mapigo kwa kuwashambulia wale waliomponda kuwapa Wachezaji wake Ofu ya Siku mbili.
Akizungumza kabla ya Jumamosi kusafiri kwenda kucheza na Stoke City kwenye Mechi ya Ligi Kuu England, Wenger amesema haamini anachosikia.
Amesema: “Tumecheza bila Mapumziko toka Desemba, hatuna haja ya kumwelezea Mtu kwamba tunahitaji kupumzika! Sielewi hawa Watu! Tumepumzika Siku mbili!”
Pia Wenger alitoboa kuwa Mesut Ozil atarejea baada ya kupona tatizo la Paja pamoja na Beki Thomas Vermaelen ambae huenda akamchezesha kama Fulbeki wa kushoto kwenye Mechi na Stoke.
Ozil, ambae alikosa Penati walipocheza na Bayern Munich, aliikosa Mechi iliyofuatia ya Ligi na Sunderland lakini Wenger amesema kukosekana kwake ni kwa sababu ya maumivu.

No comments:

Post a Comment