MSHAMBULIAJI
Lionel Messi jana aliugua Uwanja wa Taifa wa Bucharest wakati Argentina
ikilazimishwa sare ya bila kufungana na Romania.
Mshambuliaji huyo wa Barcelona alishindwa kuibomoa safu kali ya ulinzi ya Romania katika mchezo huo.
Messi aliuanza taratibu mchezo huo na ghafla akajiinamia uwanjani dakika ya saba muda mfupi baada ya kupiga mpira wa adhabu.
Baada
ya mechi, Messi akasema juu ya maradhi yake: "Hii ni hali ambayo wakati
wote inanitokea, imetokea mara chache nikiwa na Barça. Si kitu
kwangu,".
Anajisikia vibaya: Lionel Messi akiwa amejiinamia baada ya kujisikia vibaya wakati wa mchezo dhidi ya Romania jana
Messi akipasua katikati ya wachezaji wa Romania, Aleksandru Bourceanu, Aleksandru Chipciu, Mihai Pintilii na Dragos Grigore
![Catch him if you can: Messi holds off the challenge of Mihai Pintilii (right) at the National Arena Stadium](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/03/05/article-2574115-1C10189700000578-590_634x513.jpg)
Messi akimtoka Mihai Pintilii (kulia) Uwanja wa Taifa jana
![Ahead of the rest: Messi outjumps former West Ham defender Razvan Rat (right)](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/03/05/article-2574115-1C11356900000578-596_634x683.jpg)
Messi akiruka juu dhidi ya beki wa zamani wa West Ham, Razvan Rat (kulia).
No comments:
Post a Comment