Thursday, 13 March 2014

HUU NDIO UKWELI, RIHANA NA DRAKE SI SIRI TENA ..MABUSU NJE NJE...

                                                                    Kwa muda mrefu sasa kumekuwepo na tetesi za wanamuziki Drake na Rihanna kwamba wamerudisha mahusiano yao ya kimapenzi.
Ingawa wawili hao waliopachikwa jina la ‘AubRih’ (Kwa maana ya Aubrey na Rihanna) mpaka sasa wamekuwa wakisisitiza na marafiki lakini vitendo vya hivi karibuni vinaonyesha kuna kitu zaidi ya urafiki kati yao. Rihanna na amekuwa akionekana na Drake wakiongozana kwenye ziara ya kimuziki ya Drake barani ulaya.
Mara ya kwanza walionekana pamoja nchini Ufaransa, kisha Ujerumani na jana usiku walionekana pamoja jijini Manchester – England.
Na hizi ni picha za ushahidi wa wawili hao walivyokuwa wakijiachia kwenye mitaa ya jiji la Manchester usiku jana.

No comments:

Post a Comment