Jumamosi Machi 15
1800 Everton v Cardiff
1800 Fulham v Newcastle
1800 Southampton v Norwich
1800 Stoke v West Ham
1800 Sunderland v Crystal Palace
1800 Swansea v West Brom
2030 Aston Villa v Chelsea
Jumapili Machi 16
1630 Man United v Liverpool
1900 Tottenham v Arsenal
SUPA SANDE-Jumapili Machi 16
MANCHESTER UNITED v LIVERPOOL
-Old Trafford
IMEZOELEKA, kwenye Ligi Kuu England, kila Mechi hii ikifika, ni Man United ndio wanawania Ubingwa
na Liverpool ndio wasindikizaji lakini safari hii, licha ya Man United
kuwa ndio Mabingwa Watetezi, Liverpool ndio wanaowania Ubingwa na Man
United sasa wanapigania walau waingie 4 Bora.
Hii ni Mechi ya 42 kwa Man United Msimu
huu na pengine hii itakuwa mara ya 42 kwa Meneja wao David Moyes kutaja
Kikosi tofauti kwa mara nyingine tena tofauti na Liverpool ambao panga
pangua wamo Luis Suarez, Daniel Sturridge na Raheem Sterling.
TAKWIMU MUHIMU=
MAN UNITED v LIVERPOOL
VIKOMBE-Jumla:
LIVERPOOL 59 [Ubingwa England=18]
MAN UNITED 62 [Ubingwa England=20]
MECHI-Uso kwa Uso
LIVERPOOL=Ushindi 63
MAN UNITED=Ushindi 75
SARE=51
MECHI 6 ZILIZOPITA:
11 FEB 2012 Man United 2 Liverpool 1
23 Sep 2012 Liverpool 1 Man United 2
13 Jan 2013 Man United 2 Liverpool 1
1 Sep 2013 Liverpool 1 Man United 0
25 Sep 2013 Man United 1 Liverpool 0
Huku Jumatano wakikabiliwa na Mechi
muhimu ya UEFA CHAMPIONZ LIGI dhidi ya Olympiakos ambao walishinda 2-0,
ni vigumu kujua Moyes atapanga Kikosi kipi hasa kwa vile atataka
kupindua kipigo cha Bao hizo 2-0 Siku ya Jumatano.
Hata hivyo, kama alivyonena Mchezaji wa
zamani wa Man United, Gary Neville, ambae sasa ni Mchambuzi wa Sky
Sports, kwamba: “Sikubali Gemu na Olympiakos ndio yenye presha kubwa.
Nadhani hata Mashabiki wa Man United hapo Jijini kwao hawadhani kama
watafuzu UCL. Kitu ambacho Mashabiki hao hawataki ni fedheha Jumamosi au
Jumanne. Hawataki Wapinzani wao wa Jadi watue Old Trafford na
kuwaonyesha wao ni wabovu kama walivyokuwa kwenye baadhi ya Mechi Msimu
huu.”
Itakuwa kujitia kitanzi shingoni kwa Moyes kuboronga katika upangaji Kikosi.
TOTTENHAM v ARSENAL
-White Hart Lane
Tottenham na Arsenal zote zinatoka
kwenye Mechi za Ulaya zote zikiwa na vipigo na kwa Arsenal ni kubwagwa
nje ya UEFA CHAMPIONZ LIGI baada kufungwa Jumla ya Mabao 3-1 na Mabingwa
Watetezi, Bayern Munich, wakati Tottenham wamechapwa 3-1 na Benfica
kwenye Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya EUROPA LIGI.
Wiki iliyopita, kwenye Ligi, Tottenham walichapwa 4-0 na Chelsea kwenye Ligi na kuibomoa azma yao ya kumaliza 4 Bora.
Hii ni Mechi muhimu kwa Arsenal kushinda kwani Mwezi huu wanakabiliwa na Mechi nyingine nzito dhidi ya Chelsea na Man City.
No comments:
Post a Comment