MWANA DADA kutoka kiwanda cha muziki na filamu Bongo, Baby Madaha
ameonekana kukomalia kuolewa na meneja wake, Joe Kairuki huku akidai
kuwa, mwanume huyo ni mume sahihi kwake.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Baby Madaha ‘Queen of Swaga’
alisema kutokana na uhusiano wake na Joe kuelekea kwenye ndoa, mara
nyingi amekuwa akila bata zake nchini Kenya ambako ndiko mchumba wake
huyo anakotokea.
Baby Madaha katika pozi.
“Mimi sijui kwamba ni mume wa mtu kwani sijawahi kumuona huyo
mwanamke ila ninachokijua Joe ana mtoto na hajafunga ndoa na aliyezaa
naye tena wanaishi nchi tofauti kwa hiyo sioni shida kuwa naye na
mipango ya ndoa ipo,” alisema msanii huyo.
No comments:
Post a Comment