Tuesday, 18 March 2014

JUA SABABU ZA WARIOBA KUZUILIWA JANA BUNGENI

Wajumbe wa Bunge la Katiba, wakimwondoa mwenzao baada ya kutokea vurugu bungeni jana wakati Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba akijiandaa kuwasilisha Rasimu ya Pili ya Katiba. Picha na Emmanuel Herman 
******
Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta jana alipata jaribio la kwanza baada ya baadhi ya wajumbe kupinga kuruhusiwa kwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba kuwasilisha Rasimu ya Katiba kwa madai ya ukiukwaji wa kanuni za Bunge.
Wajumbe hao chini ya Umoja wa Katiba ya Watanzania (Ukawa), walitangaza mapema jana kwamba wangepinga ratiba nzima kuendelea hadi madai yao ya kumtaka Rais Jakaya Kikwete afungue Bunge kwanza kabla ya rasimu kuwasilishwa yasikilizwe.

No comments:

Post a Comment