Monday, 25 January 2016

HATIMAYE KATUMBI AAFIKI SAMATTA KWENDA GENK, KIJANA ANATUA DAR KESHO KWA SAFARI YA UBELGIJI KWENDA KUANZA MAISHA MAPYA


HATIMAYE bilionea Moise Katumbi Chapwe, Rais wa klabu ya TP Mazembe ya DRC amekubali mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ajiunge na KRC Genk ya Ligi Kuu ya Ubelgiji. Na Samatta anatarajiwa kurejea Dar es Salaam kesho kwa ajili ya safari ya Ubelgiji kwenda kuanza maisha mapya katika soka ya Ulaya. Samatta tayari amekwishasaini Mkataba wa awali na Genk wa miaka minne na sasa anakwenda kukamilisha taratibu. Samatta na Genk wanataka kukimbizana na muda ili kuwahi kabla ya dirisha dogo la usajili  halijafungwa, angalau mapema Februari Mwanasoka huyo Bora Anayecheza Afrika aanze kucheza Ubelgiji.

 
 

Meneja wa Samatta, Jamal Kisongo amesema kwamba Katumbi ameridhia Samatta aende klabu anayopenda.

Thursday, 21 January 2016

Rais Magufuli ameendelea kufanya uteuzi katika sekta mbalimbali,Na huu ndio uteuzi mpya alioufanya leo.


Alhamisi January 21 2016 ni siku nyingine ambayo Rais Magufuli kaendelea na moja ya majukumu yake kama Rais wa nchi, jukumu la leo ni kwamba kaendelea na uteuzi wa viongozi kwenye nafasi mbalimbali, uteuzi wa leo imelirudisha pia jina la Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mzee Jakaya Mrisho Kikwete.

Licha ya kusuasua uwanjani, kumbe Man United bado wako pazuri sana kifedha..liaat hii hapa


Klabu ya Real Madrid imeendelea kushika usukani kwa miaka 11 sasa katika kuingiza kiasi kikubwa cha pesa kupitia mapato yake…kwa msimu wa 2014/15 imeingiza kiasi cha Euro milioni 577.

Sunday, 17 January 2016

HIVI NDIVYO OZIL ALIVYOANGALIA MECHI YA STOKE CITY VS ARSENAL KUPITIA RUNINGA AKIWA HOME

Mesut Ozil anayeongoza kwa pasi zilizozaa mabao Premier League alikuwa nyumbani tu akiishudia timu yake ya Arsenal ikitoka sare ya bila mabao dhidi ya Stoke City.

Friday, 15 January 2016

GARI Aina ya BMW Anayomiliki Masanja Mkandamizaji Yawa Gumzo...Mwenyewe Awataka TRA Wakaikague Kama Hajalipia Ushuru

Mchekeshaji wa Orijino Komedi na mjasiriamali, Masanja Mkandamizaji amesema kila anachomiliki amekinunua kwa pesa yake halali huku akishangaa kwanini watu wameshtuka baada ya kuona anamiliki BMW yenye plate namba ya jina lake. 

Thursday, 14 January 2016

Mashabiki wa soka Ujerumani wamempigia kura Ozil na kushinda tuzo hii kwa mara ya nne …

January 14 tovuti ya timu ya taifa ya Ujerumani imetangaza jina la mchezaji bora wa kikosi cha timu ya taifa ya Ujerumani kwa mwaka 2015, tovuti hiyo imetangaza jina hilo la mchezaji bora wa mwaka 2015 baada ya mashabiki 51000 kupiga kura na asilimia 45.9 ya kura hizo kumuangukia Mesut Ozil.

Watakaoathirika kutokana na kufungiwa huko kwa Real Madrid na Atletico Madrid ni hawa wafuatao.


Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limezifungia klabu vigogo wa Real Madrid na Atletico Madrid kufanya usajili wowote hadi wakati wa majira ya koto yaani Julai 2017.

Jionee hapa Picha 30 za daraja la Kigamboni linalojengwa juu ya Bahari jijini Dar



Daraja hili linatarajiwa kukamili mwaka huu wa 2016 nakuanza kutumika.

Saturday, 2 January 2016

Achana na Lexus ya mabox, cheki na hii yenye matairi ya barafu !!(+Pichaz)


Kama kuna vitu vinayakimbiza maisha kwenye kasi ya ajabu, basi teknolojia nayo imo… uliipata ile ya Lexus iliyotengenezwa kwa mabox, ikafungwa mota alafu ikaingia barabarani na kutembea kama gari tulizozoea?

Anza mwaka kwa kutazama bonge la kichupa Odeo ft Vocaliser - Ngakukunda