Bolkiah ameanzisha kanuni mpya ya adhabu ambazo zitafanyika kulingana na mwenendo wa dini ya kiislam akisema adhabu hizi ni njia ya kufuata maamrisho ya mwenyezi Mungu ili kulinda falme yake na ushawishi unaotoka nchi za nje ambapo mara nyingi wamekua wakishawishika kupitia mitandao ya kijamii.
Adhabu zinazohusika ni pamoja na kupigwa mawe mpaka kifo, kupigwa mijeledi (floggings) na kukatwa viungo vya mwili kama miguu kwa makosa kama ya uhusiano wa jinsia moja, wizi, mimba za nje ya ndoa, unywaji pombe, kukosa kwa sala za Ijumaa, kukufuru (makosa ya lugha),ulawiti n.k na adhabu zinaweza kupungua ama kufutwa kwa wale walio chini ya miaka 18.
tume ya kimataifa ya wanasheria (ICJ) imesema sheria hizo hazitalingana na makubaliano ya sheria za kimataifa na mkuu wa tume ya haki za binaadamu UN amesema anapingana na sheria hizo.
Hoteli
hii iliyopo California Marekani ni miongoni mwa hoteli zilizosusiwa na
baadhi ya mastaa, hata wanaoandaa tuzo kubwa za dunia za Oscar wamesema
hawatofanya party hapa kama ilivyo kawaida kila mwaka wanavyofanya kabla
ya tuzo zenyewe.
No comments:
Post a Comment