KLABU ya Arsenal inapambaa dakika za
mwishoni kuelekea kufungwa dirisha la usajili
kuhakikisha inakamilisha uhamisho wa
mshambuliaji wa Manchester United, Danny
Welbeck kwa dau la Pauni Milioni 6.
Hiyo inafuatia The Gunners kumkosa
mshambuliaji wa Monaco, Radamel Falcao,
ambaye amehamia Manchester United leo.
Hivi sasa inaelezwa Welbeck anafanyiwa vipimo
vya afya Arsenal kukamilisha uhamisho huo.
No comments:
Post a Comment