Tuesday, 7 October 2014

BARCELONA KUTIMULIWA LA LIGA IWAPO KATALUNYA ITAJITENGA HISPANIA

KLABU ya Barcelona haitaruhusiwa kucheza
La Liga ikiwa Katulonya itajitenga kutoka
Hispania, Mkuu wa ligi ya nchi hiyo, Javier
Tebas amesema hayo juu ya uwezekano wa
mgawanyiko wa taifa hilo mwezi ujao.
Tebas amefafanua kwamba sheria za
michezo za nchi hiyo zinaruhusu nchi moja
tu ambayo si sehemu ya Hispania - Andorra
- kushiriki ligi hiyo au mashindano mengine,
na FC Andorra tayari inacheza katika mfumo
wa za Hispania.
Huku La Liga tayari ikionekana kuwa na
timu mbili zinazochuana vikali kwenye vita
ya mataji (pamoja na Atletico Madrid
kushinda taji msimu uliopita kuzima utawala
wa Real na Barca kwa misimu tisa)
kuwapoteza vigogo hao wa Katalunya
litakuwa pigo kubwa kwa soka ya Hispania.
Vigogo wa Hispania, Barcelona moja kwa
moja watakuwa wamejiondoa La Liga ikiwa
Katalunya litakuwa taifa huru
"Ikiwa Katalunya litakuwa taifa huru, kwa
kuzingatia Sheria za Michezo Hispania,
kwamba Barcelona haitaruhusiwa kucheza,"
Tebas, rais wa LFP, amewaambia Waandishi
wa Habari mjini Barcelona.
"Yatahitajika mabadilika katika sheri a
zilizowekwa na Bunge la Hispania. Wazi,
iwapo itatokea litakuwa pigo kubwa katika
soka ya Hispania kuwap[oteza Barca.
"Sipati picha LFP bila Barca. Kwa namna
hiyo hiyo siwezi kupata picha Katalunya bila
Hispania, Siioni La Liga bila Barca. Pia ikiwa
itatokea hivyo, utaiitaje hiyo ligi: Ligi ya
Hispania au Ligi ya Iberia?'
Sababu ambazo zimeipa Andorra fursa ya
kucheza ligi ya Hispania, nchi ndogo
kwenye milima ya Pyrenees
inayozitenganisha Hispania na Ufaransa-
zinaweza kutumika pia kuzifanya klabu za
Katalunya ziendelee kushiriki.
Barcelona, ikiwa na nyota kama Lionel Messi
katika timu yao, watabaki kucheza Ligi ya
Katalunya
Xavi na Gerard Pique ni miongoni mwa
wachezaji wa Barca waliojitokeza
kuunga mkono kung a mkono kujitenga kwa
Katalunya. Serikali ya Katalunya itaamua
Oktoba 15 juu ya mustakabali wa nchi yao.

No comments:

Post a Comment