![](http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2015/02/12/150212052220_african_migrants_italy_624x351_reuters.jpg)
Kikosi
cha ulinzi wa pwani ya Italia kimesema kimewaokoa zaidi ya wahamiaji
elfu mbili wakisafiri katika maboti katika bahari ya Mediterani-- katika
operesheni kubwa kuliko zote kufanywa kwa wakati mmoja mpaka sasa.
Meli za jeshi la wanamaji wa Italia na meli za mizigo za kibiashara pia zilizuhiska katika operesheni hiyo.
Kikosi cha walinzi wa pwani kinasema kwa mara ya kwanza walikabiliana na watu wenye silaha wanaofanya biashara ya kusafirisha watu na kuhatarisha maisha ya wafanyakazi wake.
No comments:
Post a Comment