MSHAMBULIAJI Diego Costa amepania kushinda mataji zaidi baada ya kukamilisha usajili wake Chelsea.
Mzaliwa
huyo wa Brazil, aliiwezesha Atletico Madrid kutwaa taji la La Liga
msimu uliopita, na kuifikisha Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
walipofungwa na Real Madrid.
Jose
Mourinho alishindwa kutwaa taji lolote katika msimu wake wa kwanza wa
kurejea Stamford Bridge, lakini Costa anajiamini anaweza kumsaidia
kutimiza ndoto hizo baada ya kutua magharibi mwa London.
d
"Nina
furaha sana kusaini Chelsea. Kila mtu anajua ni klabu kubwa katika livi
ya ushindani sana, na ninavutiwa sana kuanza Ligi Kuu England na kocha
babu kubwa na wachezaji wenzangu. Nikiwa nimecheza dhidi ya Chelsea msimu uliopita ninafahamu ubora wa kikosi ninachojiunga nacho,"amesema mchezaji huyo wa Hispania, anayetua Chelsea kwa dau la Pauni 32 kwa Mkataba wa miaka mitano.
Taarifa
ya Chelsea imesema; "Klabu ya Chelsea inayo furaha kutangaza kwamba
Diego Costa leo amekamilisha uhamisho wake kutoka Atletico Madrid kwa
kusaini Mkataba wa miaka mitano. Atajiunga na kikosi cha kwanza wiki
ijayo kwa ajili ya ziara ya Ulaya kujiandaa na msimu," .
MAN UNITED YANASA MAKINDA WAWILI WENYE MIAKA 15 KUTOKA BENFICA, JOAO FILIPE NA JOAO VIRGINIA KWA LENGO LA KUWAFANYIA MAJARIBIO Kimataifa
![article-0-1FA9449000000578-532_634x417](http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/07/article-0-1FA9449000000578-532_634x417-634x320.jpg)
Kinda mkali: Joao Filipe (wa pili kulia) akiwa katika gari kuelekea uwanja wa mazoezi wa Manchester United wa Carrington.
MANCHESTER United imewachukua wachezaji wawili wenye umri wa miaka 15 kutoka Benfica kwa lengo la kuwafanyia majaribio.
Winga
mwenye thamani kubwa, Joao Filipe aliwasili katika uwanja wa mazoezi
wa United wa Carrington jana jumanne na kutazamwa na makocha wa timu
hiyo.
Mchezaji mwingine aliyechukuliwa kwa majaribio ni mlinda mlango, Joao Virginia.
Mashetani wekundu watamfanyia majaribio Filipe kwa miezi sita na tayari kinda huyo alisharipotiwa kuwindwa na Barcelona.
JOAO FILIPE NI NANI?
Umri: 15
Kimo: 5ft5in
Nafasi: Winga, anaweza kucheza sehemu yoyote ya ushambuliaji
Klabu ya sasa: Benfica
Anaowapenda: Cristiano Ronaldo, Lionel Messi, Neymar
TIMU NYINGINE ZINAZOMTAKA Barcelona, Real Madrid, Chelsea, Liverpool, Arsenal
Benfica
inahangaika kuwasainisha mikataba ya muda mrefu nyota hao wawili,
lakini inakabiliana na changamoto kubwa kutoka duniani kote.
Wachezaji wengi makinda wamekuwa wakichukuliwa na United, lakini hawadumu.
Japokuwa
kwa hawa wawili, United wana msimamo wa kuwasajili mapema kutokana
na Filipe na Viriginia kuwa miongoni mwa wachezaji wakali vijana nchini
Ureno siku za karibuni.
Walipoulizwa
kuhusu wachezaji hao wawili, United walisema kamwe hawazungumzi lolote
juu ya wachezaji wanaofanya majaribio klabuni hapo.
![Hidden from view: 'The next Cristiano Ronaldo' (centre) made a low-key entrance in a Range Rover](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/07/15/article-0-1FA9449600000578-830_634x372.jpg)
MAN UNITED YANASA MAKINDA WAWILI WENYE MIAKA 15 KUTOKA BENFICA, JOAO FILIPE NA JOAO VIRGINIA KWA LENGO LA KUWAFANYIA MAJARIBIO Kimataifa
![article-0-1FA9449000000578-532_634x417](http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/07/article-0-1FA9449000000578-532_634x417-634x320.jpg)
Kinda mkali: Joao Filipe (wa pili kulia) akiwa katika gari kuelekea uwanja wa mazoezi wa Manchester United wa Carrington.
MANCHESTER United imewachukua wachezaji wawili wenye umri wa miaka 15 kutoka Benfica kwa lengo la kuwafanyia majaribio.
Winga
mwenye thamani kubwa, Joao Filipe aliwasili katika uwanja wa mazoezi
wa United wa Carrington jana jumanne na kutazamwa na makocha wa timu
hiyo.
Mchezaji mwingine aliyechukuliwa kwa majaribio ni mlinda mlango, Joao Virginia.
Mashetani wekundu watamfanyia majaribio Filipe kwa miezi sita na tayari kinda huyo alisharipotiwa kuwindwa na Barcelona.
JOAO FILIPE NI NANI?
Umri: 15
Kimo: 5ft5in
Nafasi: Winga, anaweza kucheza sehemu yoyote ya ushambuliaji
Klabu ya sasa: Benfica
Anaowapenda: Cristiano Ronaldo, Lionel Messi, Neymar
TIMU NYINGINE ZINAZOMTAKA Barcelona, Real Madrid, Chelsea, Liverpool, Arsenal
Benfica
inahangaika kuwasainisha mikataba ya muda mrefu nyota hao wawili,
lakini inakabiliana na changamoto kubwa kutoka duniani kote.
Wachezaji wengi makinda wamekuwa wakichukuliwa na United, lakini hawadumu.
Japokuwa
kwa hawa wawili, United wana msimamo wa kuwasajili mapema kutokana
na Filipe na Viriginia kuwa miongoni mwa wachezaji wakali vijana nchini
Ureno siku za karibuni.
Walipoulizwa
kuhusu wachezaji hao wawili, United walisema kamwe hawazungumzi lolote
juu ya wachezaji wanaofanya majaribio klabuni hapo.
![Hidden from view: 'The next Cristiano Ronaldo' (centre) made a low-key entrance in a Range Rover](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/07/15/article-0-1FA9449600000578-830_634x372.jpg)
No comments:
Post a Comment