Monday, 14 July 2014

SCOLARI ATIMULIWA BRAZIL BAADA YA KUWA KOCHA WA KIKOSI KIBOVU ZAIDI KIHISTORIA

KOCHA Luiz Felipe Scolari amebwaga manyanga
Brazil baada ya wenyeji hao kuboronga katika
Fainali za Kombe la Dunia mwaka huu,
wakifungwa mabao 10 katika siku tano.
Brazil ilifungwa na Uholanzi mabao 3-0 katika
mchezo wa kuwania nafasi ya tatu ikitoka
kuchapwa mabao 7-1 na Ujerumani katika Nusu
Fainali Jumanne. Hata hivyo, bado
haijathibitishwa, ni vyombo vya Habari Brazil
vimeripiti amefukuzwa.
Scolari alikutana na viongozi wa Shirikisho la
Soka Brazil Jumamosi usiku baada ya kipigo
hicho, ambacho kiliwafanya wawe kikosi cha
kwanza cha Brazil daima kufungwa nyumbani
mfululizo tangu mwaka 1940.

No comments:

Post a Comment