Monday, 14 July 2014

Full time ya Ujerumani vs Argentina, tuzo za wanasoka bora wa michuano

Baada ya mwezi mmoja hatimae michuano ya
kombe la dunia imemalizika nchini Brazil
ambapo mechi ya fainali iliwakutanisha
Ujerumani vs Argentina jijini Rio de Janeiro
kwenye uwanja wa Maracana.
Ushindi ni wa Ujerumani wa goli moja tu
lililofungwa ndani ya dakika 30 za nyongeza
baada ya full time kuwa 0-0 na mfungaji alikua
Mario Gotze aliesababisha Ujerumani kuchukua
ubingwa wake wa nne wa dunia.
Unaambiwa pia hii ni mara ya kwanza kwa
timu kutoka Ulaya kuchukua ubingwa wa dunia
kwenye ardhi ya Amerika ambapo pia kwenye
sentensi nyingine, tuzo ya mchezaji bora wa
mashindano imeenda kwa Lionel Messi,
mfungaji bora James Rodriguez, kipa bora
Manuel Neur na mwanasoka bora chipukizi wa
mashindano amechukua Paul Pogba.
MAONI

No comments:

Post a Comment