Friday, 11 July 2014

TETESI SOKA BARANI ILAYA..JUA HAPA KILA MCHEZAJI ANAENDA TIMU GANI

Kocha mpya wa Manchester United Louis van
Gaal angependa kumchukua Wesley Sneijder, 30,
kutoka Galatasaray, lakini klabu hiyo ya Uturuki
inataka pauni takriban milioni 6 (Sun), Liverpool
watamuuza Luis Suarez, 27, kwenda Barcelona
mwisho wa wiki hii, ikiwa klabu hizo
zitakubaliana ada ya pauni milioni 75 (Daily
Mirror), Lakini Arsenal wamekasirishwa kwa
sababu jaribio lao la kumchukua Alexis Sanchez,
25, kutoka Barcelona linacheleweshwa kutokana
na mkataba wa Suarez kudemadema (Daily
Express), Arsenal wanataka kulipwa pauni
milioni 6 kumuuza Mikel Arteta, 32, kwenda
Fiorentina (Times), Roma wamewapa
Manchester City hadi tarehe 21 mwezi huu
wawe wamekamilisha usajili wa beki wa kati
kutoka Morrocco Mehdi Benatia, 27, (Guardian),
Chelsea wanamsajili beki wa kulia wa Atletico
Madrid, Luis Filipe, 28, kuziba nafasi ya Ashley
Cole aliyekwenda Roma (Sun), winga kutoka
Colombia Juan Cuadrado, 27, huenda akahamia
Manchester United kutoka Fiorentina (London
Evening Standard), mshambuliaji wa Liverpool
Iago Aspas, 26, anajiandaa kuhamia Sevilla,
baada ya kushindwa kupata namba Anfield
(Daily Star), Brendan Rodgers pia anafikia kutoa
pauni milioni 10 kumchukua beki wa kushoto
wa Swansea Ben Davies, 21 (Daily Telegraph),
Manchester United, Liverpool, Chelsea na
Arsenal zitapambana kupata saini ya winga wa
Benfica Joao Filipe anayetajwa kuwa "Cristiano
Ronaldo mwingine" pamoja na kipa Joao
Virginia, wote wana umri wa miaka 15 (Daily
Express), Manchester United wanafikiria
kumsajili beki wa kushoto wa Wolfsburg na
Uswisi, Ricardo Rodriguez, 21, kuziba nafasi ya
Patrice Evra ambaye huenda akahamia
Juventus (Times), Lakini Louis van Gaal pia
huenda akamchukua beki Daley Blind, 24,
kutoka Feyenoord ikiwa Evra ataondoka
(Manchester Evening News), kiungo kutoka
Nigeria Michael Babatunde, 21, anayechezea
Volyn Lutsk nchini Ukraine, amedai kuwa
Sunderland wanataka kumsajili (Newcastle
Chronicle), Bayern Munich wamesema
wamefikia makubaliano yasiyo ya maandishi na
Atletico Madrid ya kumsajili Mario Mandzukic,
28 (Marca), mshambuliaji wa Real Madrid
Alvaro Morata huenda akajiunga na Juventus
mapema wiki ijayo (Tuttosport), na hatimaye,
kinyozi wa Alexis Sanchez amethibitisha kuwa
mchezaji huyo anahamia Arsenal! (Metro).
Share tetesi hizi na wapenzi wote wa soka.
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Cheers!

No comments:

Post a Comment