Mabingwa wa Spain, Atletico Madrid wanataka
kuwasajili Santi Cazorla, 29, kutoka Arsenal,
Fernando Torres, 30, kutoka Chelsea na
Chicharito, 26 kutoka Manchester United (Daily
Star), Chicharito amekiri kuwa hana uhakika
kama ataendelea kuwepo Old Trafford akisema
"Mungu pekee ndio anajua" kuhusu hatma yake
(Guardian), Tottenham wanatarajia kurejea na
fedha zaidi kumtaka kiungo wa Southampton
Morgan Schneiderlin, licha ya Saints kusema
mchezaji huyo hatoruhusiwa kuondoka (Daily
Telegraph), Sporting Lisbon wamewaambia
Southampton kuwa watalazimika kutoa pauni
milioni 16 kumsajili beki kutoka Argentina Eric
Dier, 20 (Daily Telepgraph), Marouanne Fellaini,
26 amekubali kujiunga na Napoli ya Italia, lakini
Manchester United wanataka pauni milioni 18
kwa mchezaji huyo aliyenunuliwa kwa pauni
milioni 27.5 mwaka jana (Daily Star), meneja
wa Sunderland Gus Poyet amethibitisha kuwa
wameanza tena mazungumzo ya kumsajili
Fabio Borini, 23, kutoka Liverpool (Daily
Express), Arsenal wanaweza kufufua
mazungumzo ya kumsajili Sami Khedira, 27,
kwa kuwa Real Madrid wanataka kumuuza
kiungo huyo (Daily Mirror), Juventus
wamekubali dau la pauni milioni 47 kutoka
Manchester United kumsajili Arturo Vidal, 27, na
mchezaji huyo wa Chile amekubali maslahi
binafsi na Old Trafford (CaughtOffside),
matumaini ya Newcastle ya kumsajili
mshambuliaji Alexandre Lacazette, 23, kwa
pauni milioni 10 yamegonga mwamba baada ya
mchezaji huyo wa Ufaransa kusaini mkataba
mpya na klabu yake (Newcastle Cronicle),
Napoli wamewapa Manchester United Dries
Mertens kubadilishana na Marouanne Fellaini
(Daily Express), Karim Benzema amekubali
kusaini mkataba mpya na Real Madrid hadi
mwaka 2018 wenye thamani ya euro milioni 7
kwa mwaka (El Confidencial), Bayern Munich
wameanza kumfuatilia winga wa Real Madrid
Angel Di Maria ambaye anasakwa pia na
Manchester United na Paris Saint-Germain
(AS). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Share
na wapenda soka wote.
Thursday, 31 July 2014
TETESI ZA SOKA ULAYA...PAUNI MILLION 47 ZAMPELEKA VIDAL MANCHESTER UNITED
Basi laua 17, kumi na mmoja watambuliwa...mashuhuda wazungumzia jinsi ilivyotokea
Wednesday, 30 July 2014
MAKOCHA WA BARCELONA WAWASILI DAR TAYARI KUTOA MAFUNZO KWA MAKOCHA WA TANZANIA
LIVERPOOL YAITANDIKA MAN CITY 3-1 MAREKANI...YAYA TOURE AKOSA PENALTI
RASMI, EVERTON WAJIBEBEA JUMLA LUKAKU KWA PAUNI MILIONI 28
DIEGO COSTA ATAKA KUZIPIGA MCHEZAJI WA VITESSE KISA KUCHEZEWA RAFU
TETESI ZA SOKA ULAYA..MAN U WAMEFIKIA MAKUBALIANO KUMSAJIRI VIDAL
Beki was Aston Villa Ron Vlaar, 29, atakuwa na
mazungumzo na meneja wake Paul Lambert
kuhusiana na hatma yake licha ya Southampton
kumwania (Daily Mirror), QPR wanafikiria
kumchukua kiungo wa Colombia Carlos
Sanchez, 28, kwa pauni milioni 4 kutoka Elche
(Daily Mirror), West Ham na QPR wamepanda
dau kwa Marseille kumchukua Matheiu
Valbuena baada ya kiungo huyo Mfaransa
kukataa kuhamia Dynamo Moscow (L'Equipe),
Manchester United na Barcelona bado
wanamfuatilia Juan Cuadrado, 26, wa Fiorentina
lakini huenda wakatishwa na bei ya pauni
milioni, 32, ya kiungo huyo kutoka Colombia
(Marca), Manchester United wamefikia
makubaliano "ya mdomo" na kiungo wa
Juventus Arturo Vidal, 27, ya uhamisho wa
pauni milioni 47 (Tuttosport), matumaini ya
Manchester City kumsajili beki kutoka Morocco
Mehdi Benatia, 27, yamefifia baada ya Roma
kusema hakuna dalili za mchezaji huyo
kuondoka (Le Figaro), meneja mpya wa
Manchester United amewaonya mashabiki wake
kuwa timu hiyo huenda ikasuasua katika miezi
mitatu ya mwanzo wa msimu wakati wachezaji
wakianza kuzoea mbinu zake (Times), Van Gaal
amesema iwapo watashinda Ligi Kuu msimu
ujao na kuwapiku majirani zao Manchester City,
utakuwa ushindi "mtamu" zaidi (Manchester
Evening News), kiungo wa Manchester City
Yaya Toure, 31, amesema huenda akasalia
katika timu hiyo hadi atakapoacha kucheza
soka (Guardian), mshambuliaji mpya wa
Barcelona Luis Suarez, 27, ambaye anatumikia
adhabu ya miezi minne, amehamia katika mji
wa Pyrenees kuanza mazoezi ya msimu mpya
akiwa na mwalimu binafsi (Daily Mail), Didier
Drogba, 36, amesema Diego Costa, 25, atakuwa
mchezaji "mkali" katika Ligi Kuu ya England
(Sun), AC Milan wanafanya mazungumzo wa
mshambuliaji kutoka Brazil Robinho, 30 (Le
Figaro), kiungo wa Arsenal Santi Cazorla,29,
bado anasakwa na Atlètico Madrid. Atlètico pia
wanamfuatilia Fernando Torres, 30, na winga
wa PSV Eindhoven Zakaria Bakkali, 18
(AS.com), kiungo anayefuatiliwa na Liverpool,
Xeridan Shaqiri, 22, huenda akaamua kubakia
na klabu yake ya Bayern Munich (Tuttosport),
Borussia Dortmund na Schalke wanamtaka
mshambuliaji kutoka Serbia, Aden Ljajic, 22,
kutoka AS Roma (Bild), Barcelona wametangaza
kumsajili kiungo kutoka Brazil, Alex Varoneze
Dione anayejulikana kama "Betri" kwa miaka
mitatu (Mundodeportivo), Manchester United
wameanza tena kumfuatilia beki wa kati wa
Atletico Madrid Miranda, baada ya Atlètico
kusema wapo tayari kupokea dau la pauni
milioni 23 (Metro), AC Milan wanamtaka winga
wa Newcastle Hatem Ben Arfa na huenda
akauzwa kwa pauni milioni 12 (Daily Star),
Bayern Munich wapo tayari kusubiri hadi Oktoba
kumsajili kipa wa zamani wa Barcelona Victor
Valdez ambaye anauguza jeraha la goti, ingawa
anaweza kusita kwenda kugombea namba na
Manuel Neuer (Mundo Deportivo), QPR
wanataka kumchukua Ronaldinho ambaye
amemaliza mkataba wake na Atletico Mineiro
(Globoesporte) na Chelsea wanakataa
kutengeneza jezi zenye jina la kipa Thibaut
Courtois, 22 na Romelu Lukaku, 22, kwa sababu
wachezaji hao bado hawajapewa namba (Daily
Star). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Share
hizi na wapenda soka wote. Cheers!!!
Monday, 28 July 2014
DUH, KUMBE DIAMOND KAWADANGANYA WATANZANIA KUHUSU KUSHINDA TUZO!!! SOMA HAPA
WASANII wa Tanzania wenye mashabiki wengi
Afrika Mashariki, Lady Jay Dee na Diamond
Platinumz, wameitoa Tanzania Kimasomaso kwa
kushinda tuzo moja moja katika tuzo za AFRIMA
(African Muzik Magazine Awards 2014),
zilizofanyika jana Dallas, Marekani.
Kwa mujibu wa mtandao wa African Music
Magazine, Lady Jay Dee alishinda tuzo ya
mwimbaji bora wa kike wa Afrika Mashariki na
Diamond Platinumz alishinda tuzo ya Msanii bora
wa kiume wa Afrika Mashariki.
Hata hivyo, kwa habari ambazo zimeenea
Tanzania na kutajwa kuwa zilizotolewa na meneja
wa Diamond zinaeleza kuwa Diamond ameshinda
tuzo mbili ambayo nyingine ni wimbo bora wa
kushirikiana.
Hali hiyo ilisababisha utata, kwa mashabiki wa
mwanamuziki huyo Diamond Platnamu hali
iliyopelekea mashabiki hao kuhisi kuwa msanii
huyo amewadanganya mashabiki wake.
Lakini kwenye orodha halisi ya mtandao a
AFRIMMA, tuzo ya wimbo bora wa kushirikiana
imeenda kwa Mafikizolo feat Uhuru (Khona).
Kwa mujibu wa maelezo aliyoandika Diamond
kwenye Instagram, inaonesha kama ameshinda
tuzo zaidi ya moja.
“First of all napenda nimshkuru sana Mwenyez
mungu, Mama, Family, My management, kipenzi
changu, Media, bila kuwasahau nyinyi mashabiki
zangu pendwa kwani sikuzote mmekuwa
mkinisupport bega kwa bega kwenye shida na
raha...Niwashkuru pia Wasanii wenzangu toka nje
na ndani ya Tanzania kwani naamini changamoto
tunazopeana ndio zimefanya hadi sasa mziki wetu
ufikie hapa...hakika tunzo hizi si zangu bali ni za
Muziki wa Bongo flavour... Mwisho kabisa
nimshkuru Mh Rais Jakaya Mrisho kikwete kwa
mchango wake wa kila siku katika sanaa yetu!...
Mr President your Son Did it!!!!! #MdogMdogo.”
Sunday, 27 July 2014
Ajali ya gari waliyoipata Waimbaji wa nyimbo za Injili akiwemo Bahati Bukuku.
RASMI, OSPINA ALIYETISHA KOMBE LA DUNIA ATUA ARSENAL
DIAMOND ANG"AA KATIKA TUZO ZA AFRIMMA 2014 MAREKANI,,AWAFUNIKA KINA T PAIN,2FACE NA WENGINE WENGI.
Zinaitwa African Muzik Magazine Awards ambapo za mwaka huu 2014 zimetolewa huko Eisemann center Texas Marekani na kuhudhuriwa na mastaa mbalimbali akiwemo Diamond wa Tanzania ambae pia alikua mmoja wa wanaowania tuzo.
Good news za ushindi wote huu ni kwa mujibu wa meneja Babu Tale ambae nae kahudhuria tuzo hizi Marekani alienitumia msg kwa kusema wametangaza ukumbini kwamba Diamond ameshinda tuzo mbili moja ya Msanii bora wa Afrika Mashariki na nyingine ni wimbo bora wa kushirikiana ambao ni ‘number one rmx’ alioufanya na Davido wa Nigeria.
Wednesday, 23 July 2014
TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA ZOTE ZIKO HAPA...CHUKUA MDA WAKL KUJUA TIMU YAKO INASAJIRI MCHEZAJI GANI ..
Meneja mpya wa Manchester United Louis van
Gaal ameambiwa kuwa anaweza kutumia kiasi
chochote cha fedha kusajili wachezaji wapya
Old Trafford na hata kuvunja rekodi za
uhamisho (Guardian), Man U Pia wametajiwa
kuwa wanaweza kuendelea kumsaka Angel Di
Maria, 26, kufuatia Real Madrid kumsajili kiungo
mshambuliaji James Rodriguez, 23, kutoka
Monaco (Independent), Arsenal wamekubali ada
ya uhamisho ya pauni milioni 3 kumsajili kipa
wa David Ospina, 25 kutoka Nice ya Ufaransa
(Guardian), boss wa Liverpool Brendan Rodgers
anataka kumsajili beki wa kulia Javier
Manquillo, 20, kutoka Atletico Madrid kwa
mkopo. Mchezaji huyo anawindwa pia na
Arsenal (Sun), Atletico Madrid wanawanyatia
wachezaji wawili wa Arsenal, Santi Cazorla na
Nancho Monreal (Daily Telegraph), Arsenal
wamerejea kumyatia kiungo wa Sporting Lisbon
William Carvalho, 22, baada ya mazungumzo ya
kumchukua Sami Khedira wa Real Madrid, 27,
kusuasua (Daily Star), Tottenham na Arsenal
wanaonesha nia ya kumsajili kiungo mshabuliaji
Douglas Costa, 23, kutoka Shakhtar Donetsk.
Mchezaji huyo kutoka Brazil amekataa kurejea
Ukraine kutokana na matatizo ya kisiasa katika
nchi hiyo (Independent), mshambuliaji Divock
Origi, 19, amesafiri kwenda Marekani
kukamilisha usajili wake wa Liverpool, lakini
atabakia Lille kwa msimu ujao (Daily Express),
uwezekano wa Didier Drogba, 36, kurejea
Chelsea huenda kukasababisha Romelu Lukaku
kuondoka Darajani, na huenda akaenda Everton
(Daily Telegraph), Everton wameripotiwa
kukaribia kumsajili David Henen, 18, kutoka
Anderlecht (Liverpool Echo), Inter Milan wako
makini kumsajili mshambuliaji wa Manchester
United Javier Hernandez, baada ya kuambiwa
na Manchester City kuwa Stevan Jovetic, 24,
hauzwi (Sun), Hull City wanazungumza na beki
wa kimataifa kutoka Cameroon Jean-Armel
Kana-Biyik, 25 kutaka kumsajili kutoka Rennes
ya Ufaransa (Sky Sports), Lionel Messi, 27,
'alitishia' kujiunga na Arsenal msimu uliopita,
wakati akizungumzia mkataba wake mpya na
Barcelona (Daily Mail), Luis Suarez, 27,
ameukimbia mji wa Barcelona, kuwaepuka
waandishi wa habari wanaomfuatilia kwa karibu
(Daily Star), Manchester United wanajiandaa
kutoa pauni milioni 39 kumchukua Arturo Vidal,
27, kutoka Juventus (Tuttosport), klabu ya
Eintracht Frankfurt ya Ujerumani imefuta
mazungumzo na mshambuliaji wa zamani wa
Arsenal Nicklas Bendtner, 26, kwa sababu
mchezaji huyo anataka mshahara mkubwa (Le
Figaro), meneja wa Borussia Dortmund Jurgen
Klopp ametupilia mbali tetesi kuwa beki Mats
Hummels, 25, anakwenda Manchester United,
na kiungo Marco Reus, 25 anakwenda Bayern
Munich (Bild), Atletico Madrid wanashindwa
kutoa pauni milioni 13 wanazotaka Chelsea
kumsajili Fernando Torres, 30, licha ya kuwa
meneja Diego Simione kutaka sana kumchukua
(AS). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Share
hizi na wapenda soka wote. Cheers!
Tuesday, 22 July 2014
DUNGA KOCHA MPYA BRAZIL, ASEMA AMEFURAHI ILE MBAYA
Hii ndio Style aliyoamua kuisherehekea B12 wa Clouds Fm kwenye Birthday yake.jionee picha hapa
Kutoka Team XXL ya Clouds Fm July 22 amezaliwa Hamis Mandi aka B12 au B Bozen ambapo Jumanne ameamua kusherehekea siku yake huu muhimu kwa kufuturu na watoto yatima.
JAMES RODRIGUEZ APIGA SHOO LA HATARI BERNABEU WAKATI AKITAMBULISHWA.. AKABIDHIWA JEZI NAMBA 10 REAL MADIRD NA
KHAMIS KIIZA ‘DIEGO’ APIGWA CHINI YANGA SC, OKWI KUENDELEA KUWIKA!
KLABU ya Yanga imembwaga
mshambuliaji wake Mganda,
Khamis Kiiza ‘Diego wa
Kampala’ baada ya kusajiliwa
kwa Wabrazil wawili, Andrey
Coutinho na Geilson Santos
Santana `Jaja`.
Baada ya Jaja kusaini
mkataba wa miaka miwili jana
makao makuu ya klabu ya
Yanga, kulikuwa na utata ni
mchezaji gani atapigwa chini
kati ya Kiiza na Emmanuel
Anord Okwi.
Awali ujio wa Jaja ulielezwa
kuwaweka kitimoto Kiiza na
Okwi, huku mmojawapo
akitakiwa kutolewa kafara.
Taarifa za uhakika ambazo
mtandao huu umezipata ni
kwamba kocha Maximo
amependekeza kuachwa kwa
Kiiza kutokana na ripoti
iliyoachwa na Hans Van Der
Pluijm.
Mzigo huo uliofuatwa chini ya
kapeti unasema kuwa Pluijm
katika ripoti yake
aliyowasilisha kwa viongozi
baada ya kumalizika kwa
msimu uliopita, alisema ili
Emmanuel Okwi acheze Yanga
sc, lazima Kiiza aondolewe.
Kwa kuzingatia mapendekezo
hayo, Maximo amefuata
ushauri huo na sasa Kiiza
rasmi anaondoka Jangwani.
Katika hatua nyingine,
imeelezwa na chanzo cha
uhakika kuwa Maximo
amewabana viongozi wa Yanga
akiwataka wajenge uwanja wa
mazoezi wa Kaunda ili
kuepukana na adhaa
anayoipata.
Maximo amewakazia na
amesema hakuna jinsi, lazima
uwanja huo ujengwe muda huu.
Pia amewataka viongozi
kuboresha vyumba vya jengo
la Jangwani ili wachezaji wote
waishe pale.
Taarifa zinasema, Maximo
amesema haiwezekani timu
kukaa saa mbili kwenye foleni
inapoelekea uwanjani na
kurudi kambini.
Kwa mazingira hayo anataka
wachezaji wake wakae makao
makuu ya Yanga, mitaa ya
Twiga na Jangwani, halafu
uwanja wa Kaunda ujengwe.
Mbrazil, Marcio Maximo
anafahamika kwa kuwa na
msimamo mkali katika mambo
yake.
MATS HUMMELS AKARIBIA KUTUA MANCHESTER UNITED!
STEVEN GERRARD-KUSTAAFU ENGLAND: ROY HODGSON, MAGWIJI WATOA MAONI!
Kuhusu miili na viungo vya Binadamu vilivyogundulika July 21 Dar es salaam.
Taarifa iliyoanza kusambaa usiku wa July 21 ni kuhusu Mabaki ya miili ya watu ambao wanasemekana zaidi ya 100 kukutwa katika msitu mdogo uliopo eneo la Mpiji,kata ya Mbweni, wilaya ya Kinondoni,ikiwa imetelekezwa.
DIEGO COSTA, FABREGAS WAFANYA VITU VYA AJABU MAZOEZINI..JIONEE HAPA
ED WOODWARD AWAHAKIKISHIA MASHABIKI MAN UNITED WAPYA WAJA!
United imetumia Pauni Milioni 50 kuwanunua Luke Shaw na Ander Herrera na kauli hii ya Woodward inaleta imani kuwa Meneja mpya Louis van Gaal atapata Wachezaji wengine wapya kabla Msimu mpya kuanza.
KUMEKUCHA ZIARA YA REAL MADRID NCHINI TANZANIA..KIINGILIO CHA CHINI NI SH 5000
Wanakuja bongo; Roberto Carlos, Ronaldo Lima, Luis Figo na Zinadine Zidane wanatarajiwa kuzuru na kikosi cha magwiji wa Real Madrid nchini mwezi ujao |
Thursday, 17 July 2014
UMAFIA HADI ULAYA, CHELSEA YAIPINDUA ARSENAL DILI LA KHEDIRA
KLABU ya Chelsea ipo kwenye nafasi nzuri ya
kumsaini Sami Khedira baada ya jana usiku
wakala wake kusema hakuna makubaliano
yaliyofikiwa na Arsenal.
Kocha wa Blues, Jose Mourinho amemsajili beki
wa kushoto Filipe Luis kutoka Atletico Madrid
kwa Pauni Milioni 18 na kuhamishia nguvu zake
kwa kiungo wa Ujerumani, Khedira.
Ilikuwa inafahamika Arsenal ilikubali kutoa Pauni
Milioni 20 kwa Real Madrid kumnunua mchezaji
huyo mwenye umri wa miaka 27, lakini walikuwa
wanasuasua kufika kiwango cha mshahara
anaotaka, Pauni 180,000 kwa wiki.
Pamoja na hayo, wakala wa Khedira, Jorg
Neubauer amesema: "Hatupo katika
mazungumzo na Arsenal. Sifikiri wanweza
kukubaliana ada, vinginevyo ningeambiwa,".
Khedira anavutiwa na Mourinho tangu
anafundisha Real na kocha huyo inafahamika pia
anampenda sana mchezaji huyo.
Wednesday, 16 July 2014
Tuesday, 15 July 2014
SAMATTA NA ULIMWENGU WAWASILI DAR NA KUSEMA; “TUTAPIGANA KWA NGUZU ZOTE KUUA MAMBA
DIEGO COSTA AMUAHIDI MOURINHO MATAJI BAADA YA KUSAINI MKATABA WA MITANO CHELSEA
MABINGWA WA DUNIA UJERUMANI WALIVYOPOKEWA KIFALME LEO NYUMBANI
Monday, 14 July 2014
BUSU LA MABUSU NI HILI LA MATS HUMMELS NA CATHY WAKE
SCOLARI ATIMULIWA BRAZIL BAADA YA KUWA KOCHA WA KIKOSI KIBOVU ZAIDI KIHISTORIA
KOCHA Luiz Felipe Scolari amebwaga manyanga
Brazil baada ya wenyeji hao kuboronga katika
Fainali za Kombe la Dunia mwaka huu,
wakifungwa mabao 10 katika siku tano.
Brazil ilifungwa na Uholanzi mabao 3-0 katika
mchezo wa kuwania nafasi ya tatu ikitoka
kuchapwa mabao 7-1 na Ujerumani katika Nusu
Fainali Jumanne. Hata hivyo, bado
haijathibitishwa, ni vyombo vya Habari Brazil
vimeripiti amefukuzwa.
Scolari alikutana na viongozi wa Shirikisho la
Soka Brazil Jumamosi usiku baada ya kipigo
hicho, ambacho kiliwafanya wawe kikosi cha
kwanza cha Brazil daima kufungwa nyumbani
mfululizo tangu mwaka 1940.
SEHEMU YA PILI .. Kauli ya Mwisho ya Ballali Kabla ya Kifo Chake
Dar na Marekani. Gavana wa zamani wa
Benki Kuu ya Tanzania BOT), Marehemu
Daudi Ballali aliacha wasia unaotaka maiti
yake isionyeshwe hadharani atakapofariki
dunia na wala maiti yake isiletwe Tanzania
kwa ajili ya maziko.
Ballali aliyefariki Mei 16, 2008 na kuzikwa Mei
23 mwaka huohuo katika makaburi ya Gate
of Heaven, eneo la Silver Spring, Maryland
nchini Marekani alifahamu kuhusu kifo chake
wiki mbili kabla, baada ya matibabu
kushindikana.
Mwandishi wa Mwananchi aliyekuwa nchini
Marekani kwa siku kumi kufuatilia suala hilo,
alibaini kuwa kiongozi huyo alilazwa mara ya
pili katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha
George Washington, April 2008 na alirejea
nyumbani kwake, Washington DC wiki mbili
kabla ya kukutwa na mauti.
Habari kutoka ndani ya familia yake
zinasema baada ya madaktari kushindwa
kumtibu walimwambia kwamba asingeweza
kuishi kwa zaidi ya wiki mbili, hivyo
walimshauri ahamie kwenye ‘hospice’
ambayo ni nyumba maalumu ya kusubiri kifo
kwa watu ambao magonjwa yao
yameshindikana.
Hospice hutumika kwa ajili ya kuwaweka
wagonjwa wanaohitaji faraja hasa kutoka na
maumivu makali chini ya uangalizi wa
washauri na wauguzi kwa lengo la
kuwaongezea wagonjwa husika siku za
kuishi.
Baadhi ya hospice hutoa huduma za kiroho,
kijamii na kifedha na wakati mwingine
huduma hizo hutolewa kwa wagonjwa ambao
wanaugulia nyumbani. Hata hivyo, gazeti hili
lilidokezwa kwamba Ballali alikataa kwenda
kwenye nyumba hiyo na badala yake kutaka
apelekwe nyumbani kwake.
“Alikataa kwenda kwenye hospice,
aliwaambia madaktari kwamba yeye hawezi
kwenda huko ijapokuwa kuna huduma nzuri
na uangalizi wa nesi (muuguzi). Aliwaambia
kwamba nitakwenda kufia nyumbani kwangu
maana nina nyumbani kwangu,” kilisema
chanzo chetu na kuongeza:
“Aliporejeshwa nyumbani, alikuwa
anazungumza kama kawaida lakini kadri siku
zilivyosogea hali ilikuwa ikibadilika na kama
sikosei siku mbili au tatu za mwisho (za uhai
wake) alikuwa anajitambua lakini alikata
kauli, hakuwa akizungumza chochote”.
Uchunguzi wetu umebaini kuwa katika siku
hizo za mwisho za uhai wake, Ballali aliacha
maelekezo kwamba pindi atakapofariki dunia,
mwili wake usiwekwe hadharani kwa maana
ya kutazamwa na watu nje ya familia wala
kusafirishwa kuja Tanzania kwa ajili ya
maziko.
“He said, he doesn’t like to be turned into a
laughing staff (alisema asingependa
kugeuzwa kichekesho), sababu watu
wasingekuja kutoa heshima za mwisho, bali
wangekuja kumdhihaki kuangalia Ballali
aliyetuhumiwa kwa ufisadi wa EPA na siyo
Gavana,” kilisema chanzo hicho.
Full time ya Ujerumani vs Argentina, tuzo za wanasoka bora wa michuano
Baada ya mwezi mmoja hatimae michuano ya
kombe la dunia imemalizika nchini Brazil
ambapo mechi ya fainali iliwakutanisha
Ujerumani vs Argentina jijini Rio de Janeiro
kwenye uwanja wa Maracana.
Ushindi ni wa Ujerumani wa goli moja tu
lililofungwa ndani ya dakika 30 za nyongeza
baada ya full time kuwa 0-0 na mfungaji alikua
Mario Gotze aliesababisha Ujerumani kuchukua
ubingwa wake wa nne wa dunia.
Unaambiwa pia hii ni mara ya kwanza kwa
timu kutoka Ulaya kuchukua ubingwa wa dunia
kwenye ardhi ya Amerika ambapo pia kwenye
sentensi nyingine, tuzo ya mchezaji bora wa
mashindano imeenda kwa Lionel Messi,
mfungaji bora James Rodriguez, kipa bora
Manuel Neur na mwanasoka bora chipukizi wa
mashindano amechukua Paul Pogba.
MAONI
Friday, 11 July 2014
TETESI SOKA BARANI ILAYA..JUA HAPA KILA MCHEZAJI ANAENDA TIMU GANI
Kocha mpya wa Manchester United Louis van
Gaal angependa kumchukua Wesley Sneijder, 30,
kutoka Galatasaray, lakini klabu hiyo ya Uturuki
inataka pauni takriban milioni 6 (Sun), Liverpool
watamuuza Luis Suarez, 27, kwenda Barcelona
mwisho wa wiki hii, ikiwa klabu hizo
zitakubaliana ada ya pauni milioni 75 (Daily
Mirror), Lakini Arsenal wamekasirishwa kwa
sababu jaribio lao la kumchukua Alexis Sanchez,
25, kutoka Barcelona linacheleweshwa kutokana
na mkataba wa Suarez kudemadema (Daily
Express), Arsenal wanataka kulipwa pauni
milioni 6 kumuuza Mikel Arteta, 32, kwenda
Fiorentina (Times), Roma wamewapa
Manchester City hadi tarehe 21 mwezi huu
wawe wamekamilisha usajili wa beki wa kati
kutoka Morrocco Mehdi Benatia, 27, (Guardian),
Chelsea wanamsajili beki wa kulia wa Atletico
Madrid, Luis Filipe, 28, kuziba nafasi ya Ashley
Cole aliyekwenda Roma (Sun), winga kutoka
Colombia Juan Cuadrado, 27, huenda akahamia
Manchester United kutoka Fiorentina (London
Evening Standard), mshambuliaji wa Liverpool
Iago Aspas, 26, anajiandaa kuhamia Sevilla,
baada ya kushindwa kupata namba Anfield
(Daily Star), Brendan Rodgers pia anafikia kutoa
pauni milioni 10 kumchukua beki wa kushoto
wa Swansea Ben Davies, 21 (Daily Telegraph),
Manchester United, Liverpool, Chelsea na
Arsenal zitapambana kupata saini ya winga wa
Benfica Joao Filipe anayetajwa kuwa "Cristiano
Ronaldo mwingine" pamoja na kipa Joao
Virginia, wote wana umri wa miaka 15 (Daily
Express), Manchester United wanafikiria
kumsajili beki wa kushoto wa Wolfsburg na
Uswisi, Ricardo Rodriguez, 21, kuziba nafasi ya
Patrice Evra ambaye huenda akahamia
Juventus (Times), Lakini Louis van Gaal pia
huenda akamchukua beki Daley Blind, 24,
kutoka Feyenoord ikiwa Evra ataondoka
(Manchester Evening News), kiungo kutoka
Nigeria Michael Babatunde, 21, anayechezea
Volyn Lutsk nchini Ukraine, amedai kuwa
Sunderland wanataka kumsajili (Newcastle
Chronicle), Bayern Munich wamesema
wamefikia makubaliano yasiyo ya maandishi na
Atletico Madrid ya kumsajili Mario Mandzukic,
28 (Marca), mshambuliaji wa Real Madrid
Alvaro Morata huenda akajiunga na Juventus
mapema wiki ijayo (Tuttosport), na hatimaye,
kinyozi wa Alexis Sanchez amethibitisha kuwa
mchezaji huyo anahamia Arsenal! (Metro).
Share tetesi hizi na wapenzi wote wa soka.
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Cheers!
JOSE MOURINHO KUMRUDISHA DARAJANI GWIJI WA CHELSEA DIDIER DROGBA
KLABU ya Chelsea inaangalia
uwezekano wa kumrudisha
Didier Drogba katika dimba la
Stamford Bridge.
Nyota huyo mwenye miaka 36
anazivutia klabu za Qatar,
wakati Juventus nao
wakifikiria kumnasa mkongwe
huyo anayecheza katika klabu
ya Galatasaray ya Uturuki.
Bado Jose Mourinho ana
mahusiano mazuri na Muivory
coast huyo na anavutiwa
kumrudisha kwa majukumu ya
ukocha zaidi.
Mkongwe huyu wa miaka 36
anazivutia klabu za Qatar, nao
Juventus wanaitaka saini
yake.
Klabu hizo za Qatar zinatarajia
kutoa ofa nono na mshahara
utajadiliwa, lakini unakadiriwa
kuwa paundi milioni 3 kwa
msimu baada ya makato ya
kodi.
Wazo la kurudi Chelsea
litaangaliwa zaidi na pande
zote.
Mourinho amekuwa na
mapenzi makubwa kwa Drogba
na anajua kuwa atakuwa na
msaada mkubwa katika kikosi
chake msimu ujao.
Alionesha nia hiyo hata
Galatasaray ilipokutana na
Chelsea katika michuano ya
UEFA mwezi machi mwaka huu
na alieleza kuwa Drogba
anaweza kurudi na yuko
makini kufanikisha hilo.
Drogba alishinda makombe
matatu ya ligi, makombe
manne ya FA na kombe la
UEFA akiwa katika klabu ya
Chelsea na Mourinho anataka
kutumia uzoefu wake
kuwashauri wachezaji wake
wapya.
Thursday, 10 July 2014
SIMBA SC YAFANYA KUFURU, YASAINI WATATU KWA MPIGO LEO AKIWEMO MANYIKA JR. NA BEKI LA MWADUI
SIMBA SC imesajili wachezaji wawili chupukizi
kwa ajili ya timu yake ya vijana chini ya umri wa
miaka 20, maarufu kama Simba B, akiwemo
Peter Manyika, mtoto wa kipa wa zamani wa
Yanga SC, Manyika Opeter.
Makamu Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange
‘Kaburu’ amesimamia zoezi hilo lililokamilika
vyema akishirikiana na Mjumbe wa Kamati ya
Usajili, Said Tuliy leo mjini Dar es Salaam.
Pamoja na kipa huyo wa timu ya taifa ya vijana
chini ya umri wa miaka 20, Simba SC pia
imemsajili kinda mwingine kutoka Mwadui ya
Shinyanga, Ibrahim Hajibu Migomba.
Kaburu maarufu kama Perez, amesema mtoto
wa Manyika amesaini miaka mitatu sawa na
Hajibu ambao wote pamoja na kusajiliwa kama
wachezaji wa Simba B, watakuwa wanakomazwa
kikosi cha kwanza.
Awali ya hapo, leo Simba SC ilimsajili kipa wa
Mtibwa Sugar ya Morogoro, Hussein Sharrif
‘Cassilas’ aliyesaini Mkataba wa miaka miwili.
Kipa huyo bora wa Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara amekuwa akiibeba Mtibwa Sugar
kwa misimu mitatu iliyopita, tangu kuondoka
kwa Shaaban Hassan Kado.
Tuesday, 8 July 2014
Watu wanane wamejeruhiwa mmoja akiwa hali mahututi kufuatia mlipuko katika mgahawa mjini Arusha
Watu wanane wamejeruhiwa mmoja akiwa hali
mahututi kufuatia mlipuko katika mkahawa mjini
Arusha Tanzania
Mlipuko huo ulitokea Jumatatu jioni na polisi
wangali wanachunguza kilichousababisha.
Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, mlipuko
huo ulitokea Jumatatu jioni na kuwajeruhi watu
wanane huku mmoja akiwa hali mahututi.
Haijulikani kilichosababisha mlipuko huo.
Kufika sasa afisaa mkuu wa shirika la ujasusi
nchini humo anakutana na wandishi wa habari.
Taarifa zaidi punde tutakapozipata.
TETESI ZA SOKA ULAYA..HAWA NDIO WACHEZAJI WANAOTARAJIWA KUAMIA TIMU HIZI..
Uhamisho wa Luis Suarez kutoka Liverpool kwenda Barcelona bado unasuasua kutokana na kutokubaliana jinsi ya kukamilisha ada ya pauni milioni 75 (Daily Mail), beki wa kulia kutoka Ufaransa Mathieu Debuchy, 28, anatarajiwa kuwa na vipimo vya afya Arsenal, akijiandaa kuhama kutoka Newcastle kwa pauni milioni 7.9 (Guardian), Newcastle huenda wakapewa Joel Campbell, 22, kama sehemu ya makubaliano ya Debuchy kwenda Arsenal (Newcastle Cronicle), Arsenal pia wanaweza kuwapa Newcastle beki wa kulia Carl Jenkinson, 22, katika makubaliano hayo (Daily Mail),
Diamond Platnumz kamzawadia hili gari mama yake leo July 07.
Wednesday, 2 July 2014
Clouds FM Kimenuka Watangazi wa Kipindi cha XXL Wapigana Live On Air
leo karibu na mwisho wa kipind cha xxl
watangazaj wa kipind hiko wamegombana
live kwenye kipind mpaka ray alipokuja na
kuwazimia mics!
kisa ni compilation album ya fiesta.
Nini maoni yako kuhusu mwenendo wao na
nani alikuwa Source au influencer wa
ugomvi?
Audio ya Ugomvi huo Coming Soon
Tuesday, 1 July 2014
HANS POPPE: F.O.S. NI UKUTA WA CHUMA, SIMBA SC SASA WAPINZANI WATAISIKIA KWENYE BOMBA
Kwa miaka mitatu sasa Simba SC haijatwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na pia haijashiriki michuano ya Afrika.
Lakini baada ya kigogo wa F.O.S., Evans Elieza Aveva kuchaguliwa kuwa Rais wa kwanza wa klabu hiyo Jumapili, Simba SC inatarajiwa kurejesha makali yake.
Mwenyekiti wa F.O.S., Zacharia Hans Poppe amesema Simba SC sasa itacheza mpira |
Kapteni wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Poppe amesema kwamba Friends Of Simba ni ukuta wa chuma.