Friday, 20 June 2014

IVORY COAST WASHUSHA PUMZI SARE UGIRIKI NA JAPAN, ILA LAZIMA WASHINDE MECHI YA MWISHO

Nenda nje: Kostas Katsouranis wa Ugiriki (katikati) akitolewa nje kwa kadi nyekundu, baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano dhidi ya Japan usiku wa kuamkia leo
 SARE ya bila kufungana kati ya Japan na Ugiriki usikua wa kuamkia leo imeongeza matumaini ya Ivory Coast kuingia 16 Bora ya Kombe la Dunia kutoka Kundi C.
Kwa safe hiyo, Ivory Coast inabaki nafasi ya kwa pointi zake tatu nyuma ya Colombia yenye poinri sita, wakati Japan na Ugiriki kila moja ina pointi moja.
Ivory Coast itamaliza na Ugiriki, wakati Japan itamaliza na Colombia, ambayo tayari imefuzu. Maana yake Ivory Coast lazima iwafunge Ugiriki kwa sababu Colombia hawatahitaji kutumia nguvu nyingi tena mbele ya Japan katika mchezo wa mwisho, zaidi kuwekeza katika mchezo wa kwanza wa mtoano.

No comments:

Post a Comment