Wednesday, 4 June 2014

RIBERY BADO HATIHATI KUCHEZA KOMBE LA DUNIA, VIJANA WAWILI WAANDALIWA KUCHUKUWA NAFASI YAKE

NYOTA wa Ufaransa, Frank Ribery bado yupo kwenye hatihati ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia katokana na kutokuwa fiti kiasi cha kutosha, ingawa kwa vyovyote Samir Nasri hawezi kuchukuliwa kuziba pengo lake hata akienguliwa kikosini.
Kiungo huyo wa Bayern Munich alitajwa katika kikosi cha mwisho cha wachezaji 23 wa Ufaransa kwa ajili ya Kombe la Dunia Brazil juzi, lakini hakuna matumaini kama atapona haraka. 
Remy Cabella wa Montpellier - ambaye wakati fulani aliwahi kutakiwa na Newcastle - na Alexandre Lacazette wa Lyon wamewekwa mkao wa kula kwa ajili ya mmoja wao kuchukua nafasi ya Ribery iwapo hatapona ndani ya muda unaotakiwa. 

No comments:

Post a Comment