Wednesday, 11 June 2014

RONALDO AITUMIA SALAMU DUNIA NZIMA "NIMERUDI", APIGA BONGE LA SOKA JANA URENO IKIUA 5-2

ILIMCHUKU sekunde 52 Cristiano Ronaldo kuithibitishia dunia kwama amepona na yuko fiti kwa Fainali za Kombe la Dunia wakati Ureno ikiitandika Jamhuri ya Irelando mabao 5-1 jana katika mchezo wa kirsfiki Uwanja wa MetLife.
Akiwa hajacheza mechi tangu baada ya Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwezi uliopita, Ronaldo aliwatoka mabeki wa Ireland baada ya kugusa mpira kwa mara ya kwaza na kufumua shuti lililolenga lango. Ulikuwa ujumbe tosha CR7 amerejea.
Mbele ya Roy Keane, mchezaji mwenzake wa zamani wa Manchester United, aligongesha mwamba, alitoa pasi, na mara mbili akakaribia kufunga na hakika alionyesha kabisa yuko tayari kwa kipute cha Brazil. Mabao ya Ureno yalifungwa na Hugo Almeida dakika za tatu na 37, Richard Keogh alijifunga dakika ya 19 na Vierinha dakika ya 77 na Fabio Coentrao na bao pekee la Ireland lilifungwa na McClean dakika ya 52.
Amerudi: Ronaldo alicheza vizuri na kuonyesha kwamba amepona na yuko tayari kwa ajili ya mechi ufunguzi dhidi ya Ujerumani wiki ijayoRaring to go: Cristiano Ronaldo was in the thick of the action as Portugal beat Ireland in their warm-up game
Shuti: Cristiano Ronaldo akifumua shut jana

No comments:

Post a Comment