Urusi imesema kwamba kikundi cha
wanajeshi wa Urusi ambacho kimekamatwa mashariki mwa Ukraine kilikuwa
kimevuka mpaka huo kimakosa huku Ukraine ikisema kwamba wanajeshi 10
walikuwa wamekamatwa.
Utawala wa Kiev umetoa mahojiano ya video ya wanaume kadhaa na mmoja wao ananukuliwa akisema hivyo si vita vyao.
Aliendelea kwa kusema kwamba watumishi wa jeshi la Ukraine walikuwa wamepita mpaka mara kadhaa lakini hawakutilia maanani kutangaza mbali waliwarudisha waliotaka kurudi Ukraine mahali palipo salama.
Msemaji wa jeshi la Ukraine Andriy Lysenko alisema kwamba hiyo haikuwa kosa mbali na kazi ya kipekee waliyokuwa wakitekeleza.
Mwanamume mmoja anayejulikana kama Ivan Milchakov anaeleza kwamba yeye huwa kwenye mji wa Kostroma nchini Urusi na anasema kwamba hakuona walipopita mpaka.
Hapo jana , vyombo vya usalama vya Ukraine vilisema wanajeshi hao wa Urusi walikamatwa wakiwa kilomita 20 kutoka mpakani ndani ya Ukraine karibu na kijiji kilichoko eneo linalodhibitiwa na waasi la Donetsk.
Rais wa Ukraine, Petro Poroshenko anatarajiwa kukutana na rais wa Urusi Vladimir Putin ikiwa ni mara ya kwanza tangu Juni, pamoja na maafisa wengine wa Umoja wa Ulaya katika mji mkuu wa Belarus, Minsk hii leo kujaribu kuutatua mzozo baina yao uliosababisha mapigano mashariki mwa Ukraine.
No comments:
Post a Comment