Friday, 1 August 2014

Wasanii wa Afrika watakaokutana na Rais Obama akiwemo Mtanzania mmoja

Screen Shot 2014-08-02 at 7.58.48 AMA.Y akiwa na wasanii wengi wakubwa kutoka Africa wamesafiri pamoja na mchezaji wa Manchester city “Yaya Toure” kwenda Washington D.C Marekani kwa ajili ya mkutano utakaofanyika kati ya tarehe 4 hadi 7 August 2014.

Safari hii ni kwa ajili ya shughuli za One Campaign ili kushiriki kutoa mchango wa kuimarisha mazungumzo kati ya serikali ya Marekani na nchi za Africa kwenye US-Africa Leaders Summit.
Rais Barack Obama atawakaribisha viongozi kutoka Africa kwenye mkutano wa siku tatu ambapo kwenye safari hii, wasanii watakuwa pia na mkutano na viongozi wa juu wa Marekani,wengine ni kutoka Young African Leaders Initiative (YALI) na members of congress.
FA Diamond Victoria Kimani na Ay wakati wa project ya One Campaign Afrika Kusini
FA Diamond Victoria Kimani na Ay wakati wa project ya One Campaign Afrika Kusini
Kwenye mikutano hii  wasanii kwa pamoja watafanya utetezi na kusisitiza wananchi wa Africa kuchukua hatua za kujihusisha na kilimo kama ONE campaign pia wasanii watafanya show kwa kuimba wimbo wa Cocoa Na Chocolate.
List ya wasanii ni A.Y. (Tanzania), Buffalo Souljah (Zimbabwe), D’Banj (Nigeria), Fally Ipupa (DRC), Femi Kuti (Nigeria), Judith Sephuma (South Africa), Omawumi (Nigeria), Victoria Kimani (Kenya) na Wax Dey (Cameroon).
Screen Shot 2014-08-02 at 8.08.54 AM 
Kwenye hii safari pia Ay amesindikizwa na mshkaji wake wa longtime Mwana FA.

No comments:

Post a Comment