BEKI
Nemanja Vidic ameaga Manchester United huku akibubujikwa damu baada ya
kugongana na mchezaji wa Southampton, Rickie Lambert timu hizo zikitoka
sare ya 1-1 katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya England.
Vidic, ambaye anaondoka United, katika mchezo wa mwisho alipewa pogo na Lambert katika harakati za kuokoa.
Kufuatia pogo hilo, mpira ukaenda kwa Steven Davis, ambaye alimtengenezea Lambert nafasi ya kufunga.
No comments:
Post a Comment