Wednesday, 30 April 2014
SAMWELI ETOO "SAMAHANI KUNA YOYOTE ANAYETAKA KUWA NYANI KAMA MIMI"
KAULI YA GUARDIOLA BAADA YA KIPIGO KUTOKA KWA REAL MADRID
MIAKA 10 YA MATUMIZI YA £830MILLION KUUSAKA UBINGWA WA 10 ULAYA
SABABU TOSHA KWA NINI RONALDO BORA DUNIA NZIMA, HAKUNA CHA MESSI WALA NANI
Monday, 28 April 2014
ANCELOTTI, GAURDIOLA WAOGOPANA KIAINA, ALLIANZ ARENA MOTO KUWAKA
CHEKI HAPA KIJANA ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUDANDIA TAIRI YA NDEGE NA KUSAFIRI MASAA 5
SENTENSI 7 MPYA ALIZOZIONGEZA JAJI WARIOBA ZINAZOHUSU KATIBA MPYA.
ADAM NDITI: MOURINHO ANATUFUNDISHA KULINDA, KUCHEZA , KUSHAMBULIA, TUTAWAFUNGA ATLETICO
Cheki picha 11 za wanamichezo maarufu enzi zao wakiwa watoto.
Kwenye picha hizi kuna watu kama Cristiano Ronaldo,Lebron James,Lewis Hamilton,Tiger Woods,Michael Owen na wengine.
WATU 683 WAHUKUMIWA KIFO MISRI.
Jaji wa mahakama nchini Misri, amewahukumu
kifo watu 683 akiwemo kiongozi wa kundi la
Muslim Brotherhood Mohammed Badie.
Mawakili wa watuhumiwa wanasema kuwa
wateja wao walikabiliwa na makosa mengi
yakiwemo, kushambulia kituo cha polisi mjini
Minya mwaka 2013 ambapo polisi mmoja
aliuawa.
Jaji huyo pia alibatilisha hukumu ya kifo
iliyotolewa kwa watu 492 kati ya watu 529.
Hukumu hiyo ilipitishwa mwezi Machi na sasa
watahudumia kifungo cha maisha jela.
Kesi na kasi ya kuzisikilizwa kwa kasi hizo,
imesababisha hasira na kukosolewa na shirika la
kutetea haki za binadamu la Umoja wa Matifa
UN.
Kadhalika shirika la Huma Rights Watch
limelalamika kuwa kesi hizo zilisikilizwa tu kwa
saa chache huku mahakama ikiwazuia mawakili
kuwawakilisha washitakiwa.
Duru zinasema kuwa jamaa wa watuhumiwa
waliokuwa wanasubiri nje ya mahakama walizirai
baada ya kupokea taarifa za hukumu hiyo.
Mwezi jana shirika la kutetea haki za binadamu la
Umoja wa Mataifa, lililaani kesi hizo likisema
kuwa zinakiuka sheria ya kimataifa ya haki za
binadamu.
Msemaji wa shirika hilo, Navi Pillay, alisema kuwa
kesi hiyo ilikumbwa na makosa mengi ya
utarataibu.
Maafisa wa utawala nchini Misri wamekuwa
wakiwasaka na kuwakamata wapiganaji wa
kiisilamu na wanachama wa vuguvugu la Muslim
Brotherhood ambao walimuingiza mamlakani
aliyekuwa Rais Mohammed Morsi ambaye
baadaye aliondolewa na Julai.
Mamia wameuawa huku maelfu ya raia
wakikamatwa.
Saturday, 26 April 2014
SNURA AKIWA KATIKA MAHABA MAZITO...MAHABA NIUE...AMKANA NGASA...CHEKI HAPA
JB APONGEZWA KUMWANIKA MKEWE
BAADA ya kuishi kwenye ndoa muda mrefu, msanii wa filamu Bongo, Jacob Steven ‘JB’ kwa mara ya kwanza amemwanika mkewe, Irene na kumwagiwa pongezi
HALIMA: KWA DIAMOND, NIPO TAYARI KUFA
DADA wa hiyari wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Halima Kimwana amejichora tatuu ya jina la staa huyo na kudai anampenda na yupo tayari kufa kwa ajili yake.
Alisema ukaribu wake ni wa kawaida lakini yupo tayari kufa badala yake (Diamond).
“Nipo tayari kufa kwa ajili ya Diamond, nimechora tatuu ya jina lake mkononi kuonesha msisitizo, namkubali” alisema Halima.
KOCHA WA BARCA TITO VILANOVA AFARIKI DUNIA..NA HII NDIO HISTORIA YAKE
Thursday, 24 April 2014
HIVI NDIVYO MASHABIKI WA MAN U WALIVYOFURAHIA KUFUKUZWA KWA DAVID MOYES KWA KUCHORA TATUU MWILINI.CHEKI PICHA.
HIKI NDICHO KIATU ALICHOVAA CHRISTIANO RONALDO WAKATI WA MECHI DHIDI YA BAYERN MUNICH NA KUVUNJA RECODI HII.
HIZI NDIZO ZAWADI ZITAKAZOTOLEWA NA VODACOM KWA WASHINDI LIGI KUU.ZAZIDI KUBORESHWA..
Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom April 24 imetangaza zawadi kwa mabingwa wa ligi kuu ya Vodacom kwa msimu uliopita ambao mabingwa walitangazwa kuwa ni Azam Fc,Ofisa Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalimu ametangaza zawadi hizi ndani ya makao makuu ya Shirikisho la Soka Tanzania TFF ambapo zawadi hizo ziko kimpangilio huu.
WARIOBA AFICHUA SIRI YA JWTZ KUHUSU MUUNGANO
HAYA NDIO MASWALI 7 YA JAJI WALIOBA KWA WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA..
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba
ameuliza maswali saba ya msingi kwa
wajumbe wa Bunge la Katiba wanaopinga
Rasimu ya Katiba iliyotolewa na Tume yake
akitaka wawajibu wananchi ili kutuliza kiu
yao.
Jaji Warioba ambaye tangu awasilishe
Rasimu ya Katiba Desemba 30, mwaka
jana amegeuka kuwa adui kwa watu
wanaotaka muundo wa serikali mbili,
aliuliza maswali hayo jana katika uzinduzi
wa ripoti ya utafiti wa Taasisi ya Twaweza
kuhusu mchakato wa Katiba.
Akizungumza kwa ukali, Jaji Warioba
alisema: "Kwanza, jibuni kwa nini
mnapinga muundo wa Muungano wakati
walioupendekeza ni wananchi?
"Sheria inasema uwepo wa Muungano na
mapendekezo katika rasimu hayasemi
Muungano usiwepo. Kumbukeni kuwa
wananchi walitakiwa kutoa mapendekezo
ya namna ya kuboresha Muungano."
Katika swali lake la pili, Warioba alisema
kwa nini Tanganyika imevaa koti la
Muungano? Kwa kuwa katika ukusanyaji
wa maoni wananchi walieleza kuwa Serikali
ya Muungano ya sasa siyo ya Muungano,
ni ya Tanganyika.
Katika swali la tatu alisema wajumbe hao
wanatakiwa kujibu maelezo ya wananchi
ambao waliieleza tume hiyo kuwa Katiba
imevunjwa na madaraka ya rais
yamechukuliwa na sasa kuna marais
wawili katika nchi moja.
"Tume inapewa lawama kubwa, wajibuni
wananchi hii tume ilitumwa na nani
kukusanya maoni ya wananchi? Waambieni
ilikusanya maoni hayo kwa kutumia sheria
ipi zaidi ya ile ya Mabadiliko ya Katiba?"
alisema Jaji Warioba katika swali lake la
nne.
Katika swali lake la tano, Warioba aliwataka
wajumbe hao kutoa sababu za kumtuhumu
kuwa amependekeza muundo wa serikali
tatu kwa sababu yeye pamoja na (Joseph
Butiku) walikuwa wajumbe wa Tume ya Jaji
Kisanga na Jaji Nyalali ambazo nazo
zilipendekeza muundo wa serikali tatu, kitu
ambacho alisema si kweli na hawakuwahi
kuwa mjumbe wa tume hizo.
Pia, aliwataka wajumbe hao kujibu swali la
sita, kwa nini hawataki kuzungumzia
yaliyomo katika Rasimu ya Katiba na
badala yake wanageuza rasimu hiyo kuwa
imeandikwa na Tume ya Mabadiliko ya
Katiba.
Katika swali lake la saba, aliwataka
wajumbe kujibu kwa nini wanaishutumu
Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa
imeingiza maoni yake, wakati ilikusanya
maoni hayo kwa mujibu wa Sheria ya
Mabadiliko ya Katiba?
Alisema badala ya kujadili hoja za msingi,
wajumbe wa Bunge hilo wamekuwa wakitoa
lugha za kejeli na matusi kwa baadhi ya
watu (akiwamo na yeye), kitendo ambacho
alisema si sahihi na kinaweza kuligawa
taifa kwa sababu yaliyomo katika Rasimu
ya Katiba yametokana na maoni ya
wananchi.
Katika uzinduzi huo walikuwepo baadhi ya
wajumbe wa Bunge hilo ambao ni Dk
Hamisi Kigwangalla aliyemwakilisha Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Julius
Mtatiro, Maria Sarungi na aliyekuwa
mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,
Humphrey Polepole.
Wednesday, 23 April 2014
HUU NDIO UJUMBE WA DIAMOND PLATNUMZ KWA MADEE...UNA MAANA NZITO SANA...SOMA HAPA
Ikiwa leo ndio kumbukumbu ya siku
ya kuzaliwa kwake raisi wa Manzese,
Madee. Tarehe 25 mwezi kama huu,
wasanii mbali mbali wametokea
kumtakia maisha marefu na wengine
kumpongeza kwa njia mbali mbali,
ila kwa hii ya Diamond Platnum ni
kali kuliko yote, Diamond ameamua
kushusha ya kwake yamoyoni kupitia
account yake ya instagram, katika
kukubali juhudi zake, kama msanii
mkongwe na kumshukuru kwa yote.
“Naamini moja ya kitu
kinachokufanya uzidi kufika mbali
na kufanikiwa zaidi ni jinsi ulivyo
na upendo kwa wasanii wote..
hususan upcoming, Nimenza
kukuskia kabla sjui lini nami
ntakuwa flani hadi leo kufikia hapa
lakini skuzote umekuwa ukinisuport
tangu naanza hadi sasa na
kunielekeza katika kazi zangu
mbalimbali… Nakuheshim sana Bro!
Happy birthday.. Mungu akupe
maisha maref yenye amani na
mafanikia tele… Eta Tudele!”
alimalizia Diamond Platnumz
REAL MADRID YAILAZA BAYERN MUNICH
Real Madrid imeibuka kifua mbele katika mechi
ya kwanza ya nusu ya fainali Ligi ya Mabingwa
Ulaya kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Bayern
Munich.
Mchezo huo umechezwa katika Uwanja wa
Santiago Bernabéu, Madrid huku bao hilo pekee
likiwekwa kimiani na mshambuliaji Karim
Benzema dakika ya 19 ya kipindi cha kwanza!
HII NDIO BARUA NZITO KUTOKA GPL KWENDA KWA LULU, UNAWEZA ISOMA HAPA
KWAKO Elizabeth Michael ‘Lulu’. Leo nimeona
nikukumbuke kupitia barua! Natambua uwezo
wako mkubwa katika kazi, juhudi zako binafsi
ndiyo zimekufikisha hapo ulipo, mataifa
mbalimbali sasa wanatambua kuwa kuna mtu
anaitwa Lulu, yupo Bongo, muigizaji!.
Sitaki kukurudisha sana nyuma lakini najua
unajua kuwa ni jinsi gani kipindi cha nyuma
ulikuwa ukipamba vyombo vya habari kwa
skendo chafu. Ulipoteza dira ya kimaisha, watu
wengi waliokuwa wakikufuatilia kazi zako
walianza kukutupa.
Walikupotezea kwa sababu ya matukio ya ulevi,
mavazi ya nusu utupu na matukio mengi ya
ajabuajabu yaliyofanana na hayo. Sina nia
mbaya kukumbusha lakini waswahili wanasema
binadamu anajifunza kutokana na makosa.
Maishani mwako umekutana na mazito
yasiyofanana na umri wako.
Kwenye ulimwengu wa mahaba, ilikuwepo
minong’ono mingi juu ya watu wanaotajwa
kushiriki mapenzi na wewe, walitajwa vigogo,
mastaa na hata wasio mastaa. Sitaki kusema ni
kweli au la lakini lisemwalo kama halipo, ujue
laja.
Siri ilifichuka kupitia kifo cha yule unayedai
alikuwa mwandani wako, marehemu Steven
Kanumba.
Mazingira ya kifo chake, umri mdogo uliokuwa
nao ilikuwa ni fundisho kubwa maishani mwako.
Ulipambana na msalaba wa gereza, ukapambana
na mlolongo wa kesi mahakamani hadi pale
ulipofanikiwa kutoka kwa dhamana, Januari
mwaka jana.
Baada ya kutoka mahabusu, kwa kipindi cha
takriban mwaka mmoja sasa ulikuwa kimya,
ulionekana kubadilika kitabia. Yale uliyokuwa
ukiyafanya awali, uliyaweka pembeni na zaidi
kusimamia mustakabali mzima wa maisha yako,
ulikuwa mwema sana aisee!.
Kinachonisikitisha ni kuanza kusikia tena matukio
ya ajabu, unaonekana kubadilika. Nimefuatilia
tabia zako, naona umeanza kubadilika,
umesahau eeeh! Mavazi yako kwa miezi
michache iliyopita, nimegundua yanaanza
kuchepuka! Mfano mzuri ni kigauni ulichokivaa
mwishoni mwa wiki iliyopita katika sherehe yako
ya kuzaliwa.
Hakikustiri maungo yako nyeti, kilionesha
sehemu kubwa ya matiti yako.
Kama hiyo haitoshi, kupitia mitandao ya kijamii
umeanza kushusha matusi mazito bila sababu
za msingi, mtu akikukosoa kidogo, unampa
maneno machafu ambayo hayaandikiki gazetini.
Kama kioo cha jamii, unapaswa kuvumilia mengi.
Nikiwa kwenye kazi zangu za kila siku, huwa
nakuwa wa kwanza kupata fununu za
mabadiliko ya kila msanii na namna anavyoishi.
Nikuonye tu, kuwa makini na mwenendo wako
kwani tayari jamii ilishaanza kujenga imani na
wewe. Uliaminika na ndiyo maana ukapata
bahati ya kuchukuliwa katika kampuni nzuri
ikakusimamia kazi zako hadi sasa.
Kwa kuwa tayari nimeanza kupata malalamiko
kutoka katika vyanzo vyangu, nikusihi sana
mdogo wangu, usirudi ulipotoka. Jenga heshima
mpya na jamii ikuamini kutokana na kazi zako
na si skendo za ajabuajabu, kwa leo ni hayo tu!
Wasalam.
NI PIGO KUBWA ..REAL HATARINI KUWAKOSA GARETH BALE NA RONALDO LEO DHIDI YA BAYERN, WOTE WAGONJWA
WINGA Gareth Bale yuko shakani kuichezaea
Real Madrid katika Nusu Fainali ya Kwanza ya
Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya mabingwa wa
Ujerumani, Bayern Munich kutokana na
kusumbuliwa nugonjwa wa mafua.
Nyota huyo wa Wales hajasafiri na wenzake kwa
ajili ya mchezo wa kwanza leo Uwanja wa
Sangtiago Bernabeu.
Kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti pia
anatilia shaka uzima wa Cristano Ronaldo.
Nyota huyo wa Ureno anatarajiwa kufanyiwa
vipimo vya afya muda mfupi kabla ya mchezo
wa leo.
Shaka tupu: Gareth Bale anasumbuliwa na mafua
kuelekea mchezo wa leo dhidi ya Bayern Munich
Ikiwa Bale ataukosa mchezo wa leo, litakuwa
pigo kwa Ancelotti, ambaye alimwagia sifa nyingi
winga huyo katika Mkutano na Waandishi wa
Habari kuelekea mchezo wa leo.
Bale anang'ara kwa sasa, baada ya kufunga bao
la ushindi katika fainali ya Copa del Rey dhidi ya
Barcelona wiki iliyopita na kocha wake akasema
mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 86
kutoka Tottenham atakuwsa mkali zaidi msimu
ujao Hispania ambao utakuwa wa pili kwake
Real.
"Gareth ni mtoto mkali,"alisema Ancelotti.
"Anavutia kwa kujiamini kiasi cha kutosha
hususan kutokana na bao alilofunga dhidi ya
Barcelona katika fainali,"alisema.
Tuesday, 22 April 2014
SABABU ZA UGOMVI BAINA YA MAPACHA WA P-SQUARE ZAFAHAMIKA, SOMA HAPA
UKWELI NDIO HUU..SIRI ZA FREEMASON ZAVUJISHWA NA BINTI WA MIAKA 16...CHEKI HAPA
David Moyes atimuliwa Manchester United
Mkufunzi mkuu na meneja wa klabu ya
Manchester United David Moyes ametimuliwa.
David Moyes amefutwa kazi baada ya kushikilia
usukuni wa klabu hiyo kwa miezi kumi tu.
Klabu hiyo hapo awali ilikuwa imekataa
kuzungumzia udaku wa magezti kuwa Moyes
atafutwa kazi kabla ya msimu kumalizika.
Moyes, mwenye umri wa miaka 50, aliteuliwa na
Ferguson kumrithi alipostaafu mwaka jana baada
ya kuwa na klabu hiyo kwa miaka 26.
Taarifa kutoka kwa klabu hiyo imemshukuru
Moyes kwa bidii, uaminifu na hekima
aliyoonyesha kocha huyo akiwa mkufunzi wa
Manchester United.
Moyes alichukuwa usukani wa kuifunza
Manchester United mwaka uliopita baada ya
aliyekuwa kocha wa siku nyingi Sir. Alex
Ferguson kustaafu.
Huku zikiwa zimesalia mechi nne pekee msimu
wa ligi kukamilika Mancheseter united inashikilia
nafasi ya saba kwenye jedwali la msimamo wa
ligi hiyo alama ishirini na tatu nyuma ya viongozi
Liverpool.
Klabu hiyo imeshindwa kufuzu kushiriki michuano
ya ligi ya mabingwa ulaya kwa mara ya kwanza
katika kipindi cha takriban miaka ishirini.
Monday, 21 April 2014
BREAKING NEWZZ! MOYES KIBARUA CHAOTA NYASI MAN UNITED
KUNA taarifa zimezagaa kuwa kocha wa
Manchester United, David Moyes
amefukuzwa kazi, japokuwa
haijathibitishwa na familia ya Glazer ambao
ndio wamiliki wa klabu hiyo.
Inasemekana familia ya Glazer imefikia
maamuzi ya kumfukuza kazi bosi huyo wa
Man United ikiwa ni miezi 11 tu tangu
arithi mikoba ya Sir Alex Ferguson.
Msemaji wa Man United amegoma kueleza
kama kweli Moyes amefukuzwa kazi, lakini
imefahamika kuwa kocha huyo hatakuwepo
katika mchezo ujao dhidi ya Nowrich City
kwenye uwanja wa Old Trafford jumamosi .
Kocha mchezaji Ryan Giggs anatarajiwa
kuiongoza Man United mpaka mwishoni
mwa msimu, na wakati huo huo wasaidizi
wa Moyes Steve Round, Phil Neville na
Jimmy Lumsden pia wanatarajiwa
kuondoka na bosi wao.
Kocha wa kudumu wa Mashetani wekundi
anatarajiwa kutangazwa mwishoni mwa
msimu huu.
Familia ya Glazer amechukizwa na kipigo
cha jana cha mabao 2-0 dhidi ya Everton
na kuwa mechi ya 11 kwa Man United
kupoteza katika mashindano yote mwaka
huu.
Moyes alisaini mkataba wa miaka 6 mwezi
mei mwaka jana kurithi mikoba ya Sir
Ferguson aliyestaafu, lakini ameshindwa
kupata mafaniko.
Baada ya familia Glazer kufahamu kuwa
Man United haitamaliza ligi katika nafasi
nne za juu, wameamua kuotesha nyasi
kibarua cha Moyes.
Man United wanaelekea kuwa mabingwa
watetezi waliofanya vibaya zaidi katika
historia ya ligi kuu England kwa kuwa
nafasi ya 7 na kwa mara mwisho Ray
Harford alifanya hivyo na Blackburn Rovers
mwaka 1996. Pia wanatarajia kukosa hata
ligi ya Europa msimu ujao.
Bodi ya ukurugenzi ya Man United imekuwa
ikimvumilia Moyes kwa matokeo mabaya,
lakini walikerwa sana hasa walipofungwa
nyumbani na wapinzani wao wakubwa
Liverpool na Manchester mwezi uliopita.
WAANDISHI WA HABARI WAISHI MIEZI 6 GIZANI NA MIEZI 2 NA NUSU WAKIWA WAMEFUNGWA MINYORORO BAADA YA KUTEKWA..
Wanahabari wanne wa Ufaransa walioachiliwa
baada ya kutekwa nyara na wanamgambo nchini
Syria karibia mwaka mmoja uliopita wamewasili
nchini Ufaransa.
Waandishi hao wamekuwa wakisimulia masaibu
yao walipokuwa mikononi mwa watekaji wao
wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa kiisilamu
wenye uhusiano na kundi la Al Qaeeda.
Mmoja wa waandishi hao, Didier Francois,
alisema kuwa walifungwa kwa minyororo kwa
pamoja na kufungiwa katika chumba kisicho na
mwangaza
Mwenzake Nicolas Henin, alisema kuwa watekaji
wao hawakuwatendea vizuri.
Bwana Henin na Francois wakiandamana na
Edouard Elias na Pierre Torres, waliamkuliwa na
familia zao pamoja na Rais Francois Hollande
walipowasili nchini Ufaransa.
Kuokolewa
Walipatwa na wanajeshi wa Uturuki wakiwa
katika mpaka wa Syria na Uturuki
Kundi la wapiganaji la 'Islamic State of Iraq' lenye
uhusiano na kundi la Al Qaeeda limetuhumiwa
kwa utekaji huo.
Picha za wanaume hao ziliwaonyesha wakiwa
wamechakaa ingawa walikuwa bukheri wa afya.
Bwana Francois,mwenye umri wa miaka 53,
alisema alikuwa na furaha sana kwani yuko huru,
ameweza kuona mbingu, kutembea na
kuzungumza bila kikwazo chochote.
"tuliishi kwa miezi sita gizani huku miezi miwili
na nusu tukiwa tumefungwa kwa minyororo,''
aliambia kituo kimoja cha redio anachokimiliki.
"tuliona siku ndefu , ingawa hawakuwahi
kupoteza matumaini,'' aliongeza bwana Francois.
Waandishi hao walipatikana wakiwa
wamefunikwa nyuso zao na kufungwa minyororo
katika sehemu moja ya mpakani mwa Syria na
Uturuki.
Waliokolewa na wanajeshi wa Uturuki.
Wanaume hao walitoweka katika matukio mawili
tofauti mwezi Juni mwaka jana.
Bwana Francois, ni mwandishi mwenye uzoefu wa
miaka mingi na Elias ni mpiga picha. Wote
walitekwa nyara wakielekea mjini Aleppo.
Henin, alikuwa anafanya kazi na jarida la Le Point
huku bwana Torres, akiripotia kituo cha
televisheni cha channel Arte, walitekwa nyara
baadaye mwezi huo karibu na eneo la Raqqa.
Zaidi ya waandishi 60 wameuawa nchini Syria
tangia kuanza kwa mgogoro dhidi ya serikali ya
rais Bashar al Asaad miaka mitatu iliopita.
UKWELI NDIO HUU..MILLIONI 13 ALIZOZITOA WEMA SEPETU KUMUOKOA KAJALA KWENDA MAHAKAMANI AZIKUA PESA ZAKE..
Siri
zimezidi
kuvuja juu
ya
uhasama
baina ya
mastaa wawili wa
kike bongo.
Miss tanzania 2006. Wema sepetu na
kajala masanja. Ambapo inaelezwa
kuwa kiasi cha pesa sh.mil 13.
Ambazo wema alimlipia kajala
kumuokoa na hukumu ya kwenda
jela katika mahakama ya hakimu
mkazi kisutu dar hazikuwa zake.
kwa mujibu wa watu wa karibu na
mastar hao Wema hakuwa na jeuri
ya kutoa fedha hizo ndio maana
familia ya mrembo huyo ilionyesha
mshtuko mkubwa kwa binti yao
kutoa pesa za bure kwa mtu baki
kama kajala.
Habari zaidi zimesema kwamba
kabla wema hajatoa pesa hizo
alimpigia simu mfadhili huyo na
kumueleza kilichokuwa kinaendelea
mahakamani hapo ambapo aliruhusu
pesa kutolewa.
kama pesa hiyo ingetoka mfukoni
mwa wema basi familia yake
akiwemo mamake asingeweza
kumwacha bila kumuhoji bint
yake.lakini mama wema
alieleweshwa hali ilivyo na ndio
maana akatulia.pesa ilitolewa na
kigogo huyo ambaye sasa anatoka na
kajala.
Aidha mtoa habari huyo alidai
kwamba kabla ya wema kumsaidia
Kajala mil.13 hakuwahi kutoa
msaada wowote wa kifedha zaidi ya
kula ubwabwa na watoto yatima.
Sani iliwahi kumpa taarifa wema
kwamba kulikuwa na mama
anayehitaji msaada wa laki moja
kutokana na matatizo aliyokuwa
nayo alijibu kwamba yeye sio
serikali na kumsaidia Kajala
kusiwafanye watu wamuone kama
taasisi ya kutoa misaada.
Taarifa zaidi zimedai kwamba
kutokana na tabia za mastaa zilivyo
isingekuwa rahisi kwa Wema kutoa
hata senti tano yake!
Naamini kwa hali ya mastaa ilivyo
Wema kama wema asingeweza kutoa
hata sh. Mia ili kumtoa kajala.Nyuma
ya kesi ya kajala kulikuwa na huyo
kigogo ambaye hivi sasa pesa zake
zote anammwagia kajala.mambo
yamegeuka ndivyo sivyo!” alisema.
Vyanzo vyetu hivyo vilitoa mfano wa
msanii mwingine jack wolper
ambaye alimpa msaada wa mil.10
aliyekuwa nyota wa filam Juma
kilowoko au Sajuki kwa ajili ya
matibabu na kudai hazikuwa zake ,
Wolper hakuwa na uwezo huo pesa
zilikuwa za Dallas ambaye alimtumia
Wolper kama kama bahsha
kuufikisha mchango wake. Kiliongea
chanzo hicho.
# BREAKINGNEWS:ZAIDI YA WATU 20 WAMEFARIKI DUNIA KWA AJALI YA GARI..
Zaidi ya watu 20 wamefariki
dunia papo hapo na wengine wengi kujeruhiwa
baada ya basi la LUWULE walilokuwa wakisafiri
nalo kutoka Musoma kwenda Mwanza kuacha
njia,kugonga nyumba na kupinduka katika kijiji
cha Itwimila wilaya ya Busega.Kwa habari zaidi endelea kutembelea Kitomixnews uweze kujua.
Sunday, 20 April 2014
HII NI KWAAJILI YAKO MWANAUME. Jinsi ya kujua kama umemfikisha kweli au anakuibia na kukushika masikio kwa kelele za kimahaba.
Mimi sio mwigizaji, zaidi ya hapo nilikuwa
mtu wa mwisho kwenye maigizo kipindi cha
shule ya msingi, ila nina uwezo mkubwa wa
kusema "Oooh, hapo hapo.. unanifikishaaa!",
mpaka mwanaume akahisi kweli
amenifikisha, hata hivyo siko peke yangu
wanawake wengi tu wanaigiza wakati wapo
wanafanya mapenzi.
Utafiti wa kitaifa wa ngono uliofanywa na
chuo cha indiana, ulionyesha asilimia 85% ya
wanaume wakisema mara ya mwisho
kufanya ngono waliwafikisha kileleni wenza
wao, hata hivyo asilimia 64% tu ya
wanawake walisema walifika kileleni mara ya
mwisho walipofanya ngono, hii inamaanisha
ni hesabu ya ajabu hata mtoto wa darasa la
pili anajua imekosewa, na inamaanisha
asilimia 21% ya wanaume walidanganywa na
milio ya kimahaba ya wenza wao na
wakaamini kuwa waliwafikisha.
Iwapo tukichukulia na wewe utaki kuwa
mmoja wa hao waliodanganywa na mbaya
zaidi hawakua na ufahamu wowote kuwa
wamedanganywa, waulize wanaume
wamekuandalia dalili zinazoonyesha na
zitakazokuwa zinakuonyesha iwapo
unadanganywa.
Tuweke hivi, "Ooooh, hapo hapo usiitoe...
ooh, naisikia mpaka kichwani!", mwanamke
huwa anasema hivi akiwa anakandwa miguu
yake na maji ya moto baada ya safari ya
miguu ya mwendo mrefu, "OH... USI....,
JAMA... UNA.... NDIO...., HAPO HA...", hivi
ndomwanamke anavyosema ukiwa
unashughurika vizuri kitandani, akiweza
kuunganisha sentensi nzima na ikaeleweka
ujue anakuzuga, maana akifikia mshindo akili
yote inakua kama haifanyi kazi vizuri na
ikitokea akiwa analia kama kwenye video za
ngono wanavyolia, ujue anakusubiri umalize
mambo yako aanze kukuelezea shida zake
alizonazo, wale wa kwenye video za ngono
huwa wana igiza, mwanamke wa kihalisia wa
kawaida huwa hawafiki kileleni iwapo
mwanaume anatumia nguvu ovyo ovyo bila
ya mpangilio na msuguano wowote
unaohusisha kinembe.
Kwa mwanamke ili afike mshindo, inabidi awe
na umakini mkubwa na kuweka hisia zake
zote kwenye msuguano na msisimko
anaoupata mwilini mwake ili afike mshindo,
kubusu na kutekenya hawezi kuvifanya kwa
wakati huo ambao anaweka mawazo yote
mahala hapo, ukiona unataka kumpiga denda
akageukia pembeni ujue mambo ndo
yamemkolea vizuri na sio vinginevyo.
Ulishawahi kujiangalia kwenye kioo wakati
uume wako unagombana na mikono yako,
najua ulishawahi kujisugua, nani ambae
hajawai..., hakuna!, na unaelekea yale
mambo kumwagika, unajua usowako
unakuwaje?, uso wako unakuwa kama vile
unataka kutolewa maisha au kama unataka
kulia vile, binadamu wote wako sawa upande
wa kihisia, hata wanawake pia!, akiwa na
sura nzuri wakati ndo anafika mshindo ujue
hapo hakuna!, anatakiwa kuwa na sura
ambayo haina mvuto kama anataka kulia na
sio awe bado anapendeza kama ndo anaingia
harusini.
Mwanamke kufika kileleni kwa stairi ya
kutoka kwa nyuma ni sawa na wewe kufika
mshindo huku mwanamke akiwa anakuchzea
kwa mikono.
Sijasema haiwezekani, ila inahitaji ufundi
mkubwa na dereva inabidi awe anaijua kwa
umakini mkubwa njia yake anayopita, ili
manbo hayo yaweze kutokea, kwa hio
nitakua na wasiwasi kama mwanamke
akisema kafika kileleni kwa kutumia hio
stairi, mwanamke anauwezo mkubwa wa
kufika kileleni iwapo anafanya mapenzi ila
yeye ndo yuko juu ya mwanaume kashika
msukani, au kwa stairi ya missionary
inayoitwa Coital Alignment Technique kwa
kifupi The Cat, najua huijui... i gugo(google)
na utaiona.
Mwanamke akiwa amefika kileleni, moyo,
presha ya damu na mdundo vyote vinakuja
juu ambavyo inamaanisha lazima jasho
limtoke kwa aina yeyote ile na mwili unakua
na majimaji kwenye ngozi, hii ni moja ya
dalili amekwea mlima na kufika kileleni kwa
furaha
at
Unahisi unaweza kutofautisha kama
umemfikisha kweli au anapiga kelele
za kimahaba za kukuzingua?,
mwanamke ambaye zamani alikua
anamzingua mpenzi wake kwa
kelele za kimahaba anatuelezea
kwanini ni vigumu kuliko unavyofikili
kutambua na utatambuaje!.
#1; Unamwelewa
#2; Anakubusu bila kuacha
#3; Uso wake unakuwa mzuri
#4; Unafanya mapenzi na mpenzi wako
kwa stairi ya kimbwa mbwa
#5; Ngozi yake inakuwa nyororo na kavu
Saturday, 19 April 2014
NI NGUMU KUAMINI LAKINI BAADA YA MIAKA 10 HATIMAYE HUU NDIYO MWISHO WA KUNDI LA P-SQUARE KUTOKA NCHINI NIGERIA.....!!!
I've been hearing a few stories about Peter
and Paul Okoye of P-Square having issues for
a while now. I hear they disagree on
everything now...songs, videos, ideas
etc...but because they are twin brothers, I
figured well, they will sort things out...so I
didn't write.
On Wednesday April 16th, I gathered
exclusively from industry sources that the
brothers fought each other physically during
rehearsals. They had to be separated by their
dancers. This is fact! But I decided to leave
the story alone because which sibling doesn't
disagree sometimes, right? But now their
older brother, Jude Okoye, who is also their
manager, just tweeted that after ten years
he's done.
I hear one of
the wives is
causing some of the problems between the
brothers. *sigh* Dear P-Square, don't even
think of breaking up. You will break the
hearts of millions of people...including
myself. Please stay together.
credit : hot news daily
JERR SILAA" YANGA HAKUNA KUJENGA UWANJA JAGWANI ..PALE NI MKONDO WA MAJI"
Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa
amepigilia msumari wa mwisho kwa kuwataka
Yanga kusahau kuhusu ongezeko la eneo la
kujenga uwanja wake eneo la Jangwani kwa vile
sehemu hiyo ni mkondo wa maji.
Akizungumza na gazeti hili, Dar es Salaam jana,
Silaa alisema:
“Tumepata hasara kubwa (Serikali) hii yote
imetokana na watu kujimegea maeneo na
kujenga kwenye mkondo wa maji, mafuriko yote
haya yanayotokea ni kwa vile maji yanakosa pa
kwenda na kuishia kwenye maeneo mengine
ndiyo maafa yote haya yanatokea.
“Hebu angalieni pale Jangwani sasa hivi kulivyo,
maji yamefurika watu wengine wamepoteza
maisha, halafu bado turuhusu watu waendelee
kujenga kwenye mkondo wa bahari, waambieni
wasahau hilo.”
Kauli hiyo ya Meya Silaa imekuja siku chache
baada ya Baraza la Mazingira la Taifa (NEMC)
kudai kuwa eneo ambalo wanaliomba Yanga ni
hatarishi, hivyo watafute eneo lingine kwa ajili ya
ujenzi wa uwanja wao kama kweli uongozi uliopo
chini ya Mwenyekiti wake, Yusuf Manji, una nia
ya kuwajengea Wanayanga uwanja.
Eneo hilo la Jangwani, mbali ya kuwa ni bonde
kubwa la Mto Msimbazi, ambalo ni mkondo wa
upumuaji wa bahari, lakini pia kuna bomba
kubwa linalopeleka maji Hospitali ya Taifa
Muhimbili na lingine linalopeleka maji taka
baharini.
Hata hivyo, licha ya Yanga kushauri kuondoka
eneo hilo ambalo ni hatarishi, uongozi wa klabu
hiyo chini ya Mwenyekiti wake wa
Ujenzi wa Uwanja, Francis Kifukwe, umezidi
kusisitiza kuwa kuna masharti ambayo NEMC
wamewapa na wakiyatimiza eneo hilo watapewa
ikiwemo kubeba fidia za kuwalipa wakazi wa
eneo hilo.
“Kuna masharti ambayo wametupa na sisi tupo
tayari kuyatekeleza hawajatuambia chochote,
huyo aliyekwambia tumenyimwa kujenga uwanja
ni nani? Nitajie huyo mtu wa NEMC,
ninachoweza kusema kuna masharti na
maelekezo ambayo wametupa,” alisema Kifukwe
huku akigoma kuzungumzia suala hilo kwa
undani kwa kueleza masharti na mapendekezo
waliyopewa.
Kamati ya Mipango Miji na Mazingira ya
Manispaa ya Ilala ilikutana hivi karibuni kujadili
suala hilo ambalo hata hivyo wameliacha
mikononi mwa NEMC.
Nayo Kamati ya Mipango Miji na Mazingira ya
Manispaa ya Ilala ilifanya ziara ya ukaguzi wa
Jangwani hivi karibuni
Wakati huohuo; Mvua hizo zinazoendelea
kunyesha zimesababisha ukuta mkubwa wa uzio
wa uwanja wa Yanga, ambao umejaa maji kwa
sasa kubomoka. Ukuta huo ni ule ambao upo
upande wa bonde la Msimbazi chini ya uwanja
huo.
Thursday, 17 April 2014
SASA KILA KITU WAZI MSANII JUX ATUMIWA NA FREEMASONRY~ USHAHID HUU HAPA
zikivuja siku hadi siku. Mingoni mwa siri zao hizo ni nembo ambazo zimekuwa zikiwawakilisha zikiwa na maana ya kumpinga Mungu na kumpa sifa shetani.
WAZIRI LUKUVI AWALIPUA CUF.."CUF WANASHIRIKIANA NA UAMSHO"
KUMBE NAHODHA WA KIVUKO KILICHOZAMA HAKUWA KWENYE USUKANI.
IJUE HAPA LISTI YA WASANII WA HIPHOP WENYE PESA NYINGI DUNIANI,,50 CENT AZIDI KUSHUKA
MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR NAE AUNGANA NA UKAWA ASEMA SEREKALI TATU NDIO MPANGO MZIMA
MAN CITY YALAZIMISHWA SARE YA 2-2 ETIHAD NA SUNDERLAND
Huyu hapa; Kinda aliyeifungia Sunderland mabao mawili leo,Wickham akishangilia |
RONALDO NA REAL MADRID WALIVrOJIRUSHA NA NDOO YA MFALME JANA.
KAULI YA MBOWE KUHUSU UKAWA KUSUSIA BUNGE
Mheshimiwa Mbowe ameeleza jinsi ambavyo bunge linavyoendeshwa kwa upendeleo mkubwa sana,Matusi makubwa ya nguoni kwa wajumbe wenye mawazo tofauti na ya serikali ya ccm,kutumia vitisho vingi,udhalilishaji na uonevu mkubwa .
Wednesday, 16 April 2014
ALICHOKISEMA WAKALA WA MCHEZAJI TONI KROOS KUHUSU KUHAMIA MAN UNITED.
Tetesi za usajili wa mchezaji wa FC Bayern
Munich Toni Kroos zimezidi kutengeneza
vichwa vya habari katika media.
Wakati mapema wiki hii kocha wa Bayern Pep
Guardiola akisema kwamba hatma ya mchezaji
ipo mikononi mwake mwenyewe, leo hii wakala
wake amezungumza na kauli inayoonyesha
mchezaji huyo anaweza kubaki Bayern Munich
mpaka mkataba wake utakapoisha mnamo
2015.
Muda mfupi baada ya Guardiola kusema
kwamba hatma ya mchezaji ipo mikononi
mwake mwenyewe, gazeti la Guardian la
Uingereza likaripoti kwamba Manchester United
imempa ofa ya mshahara wa paundi 260,000
kwa wiki, fedha ambayo itakuwa ni mara nne
ya anayopata sasa 72,000 pounds kwa wiki.
Lakini leo Jumatano wakala wa mchezaji
huyo Volker Struth, amesema United
haijawafuata rasmi kuhusu suala la kutaka
huduma za mchezaji huyo.
Alisema: “Hakuna ofa rasmi ya mkataba na
Bayern. Pia zaidi sidhani kama kuna hitaji la
kutoa ofa mpya, kwa sababu Toni Kroos
ataendelea kuichezea Bayern mpaka 2015.”
Wakala huyo ameshaonekana akiwa pamoja na
kocha United David Moyes takribani mara mbili
katika miezi ya hivi karibuni.
KAULI YA AZAM FC JUU YA TUHUMA ZA KUNUNUA UBINGWA WA VPL.
Zikiwa zimepita takribani siku nne tangu Azam
FC ilipoandika historia ya bingwa wa mpya wa
ligi kuu ya Vodacom huku tetesi zikizidi
kuzunguka mitaani kwamba klabu hiyo ya jijini
Dar es Salaam imekuwa ikihonga sana
wachezaji wa timu nyingine pamoja na marefa
ili kujihakikishia ushindi na hatimaye kutwaa
ubingwa kabisa.
“Maneno yanayozungumzwa ni porojo Baada
ya Azam Fc kupata mafanikio ya kuwa bingwa
wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Azam Fc ilipata
nafasi ya pili mara Mbili katika Ligi Kuu ya
Tanzania bara haikuwai kusemwa imenunua
leo iweje imekuwa Bingwa isemwe imenunua.
John Bocco ameweka Historia Baada ya
Kufunga Goli la Ushindi ktk Mechi ya Mwisho
ya Ligi Daraja la kwanza na Kuipandisha
Azam Fc kucheza Ligi kuu ya Tanzania Bara,
na leo Hii Tumeshuhudia John Bocco ameweka
Historia ya Kufunga Goli la Ushindi na Kuipa
Timu ya Azam Fc Ubingwa kwa Mara ya
kwanza Tangu ilipopanda Daraja kucheza ligi
kuu ya Tanzania Bara kwa Msimu 2013/2014
na kucheza Bila kupoteza hata mechi Moja.
Hatuto puuzia mechi ya mwisho Dhidi ya JKT
Ruvu Tutacheza kama mechi nyingine
Tulivyocheza Tunahitaji kuweka Historia ya
Kutokupoteza hata Mechi Moja kwa Msimu
Huu JKT Ruvu wajiandae kwa Kichapo wakati
Tukiwa Tunakabidhiwa Kombe letu la Msimu
Huu
Baadhi ya Maneno ambayo Makocha
wanazungumza Sio Mazuri wao kama
wataalam hawatakiwi kujihusisha katika
Propaganda ambazo baadhi ya watu
wanaziendeleza.”
DIAMOND ATOBOA SIRI KUWA ANA MTOTO..CHEKI PICHA
Kwenye mahojiano hayo, mtandao huo ulimuuliza: What have you learnt about fatherhood, now that you’re a father (umejifunza nini kuhusu ubaba kwakuwa sasa wewe ni baba)
DIAMOND ATOBOA SIRI KUWA ANA MTOTO..CHEKI PICHA
Kwenye mahojiano hayo, mtandao huo ulimuuliza: What have you learnt about fatherhood, now that you’re a father (umejifunza nini kuhusu ubaba kwakuwa sasa wewe ni baba)
Tuesday, 15 April 2014
BINTI WA ADVANCED LEVEL ANANIKOSESHA RAHA NDANI YA NDOA YANGU
KABLA GURUMO HAJAFARIKI ALIMWANDIKIA DIAMOND WIMBO KAMA ZAWADI .
Diamond alimzawadia mzee Gurumo gari mpya mwaka jana wakati wa uzinduzi wa video yake ya ‘Number 1’.
MAN CITY YAFUNIKA KLABU ZOTE DUNIANI KWA KULIPA MISHAHARA MIKUBWA, HAKUNA CHA BARCA WA REAL
KUTANA NA MAPACHA WANAOCHANGIA KILA KITU MPAKA BOYFRIEND WAO NI MMOJA.
SEIF SHARIFF HAMAD KAZUNGUMZA LEO, KAULI ZAKE 7 KUHUSU MUUNGANO ZIKO HAPA...
Amekua mmiliki wa vichwa vya habari
kutokana na ripoti mbalimbali ambazo zimekua
zikimnukuu kwa kudai kutozitaka serikali mbili
lakini leo April 15 2014 amezungumza kwenye
maonyesho ya miaka 50 ya muungano ya
kuzitoa hizi kauli zifuatazo.
1. ‘Pamoja na milima na mabonde, muungano
huu umedumu miaka 50, nchi nyingine
zilishindwa, l azima tufanye tathmini hasa ya
muungano wetu, lazima vijana waelimishwe vp
muungano uliundwa, tulianzia vipi’
2.‘Ukitaka upate maenedeleo, yatambue
mafanikio yako lakini pia usisahau matatizo
yako, ni ni moja.. kufanya vizuri, Sidhani katika
Tanzania kama kuna watu hawataki muungano,
na kama wapo ni wachache, muungano
uendelee ndio la msingi’
3. ‘ Sio dhambi watu kuwa na fikra tofauti, sio
dhambi hata kidogo kwa sababu hatuwezi wote
kuwa na fikra aina moja, Wanaotaka serikali
moja wasibezwe, mbili wasibezwe, wanaotaka
tatu na serikali ya mkataba wasikilizwe pia’
4. ‘ Wako wanaoamini kwamba matatizo ya
muungano yako kwenye muundo, tuwasikilize
wana hoja gani, Mwaka 1963 Malaysia na
Tanganyika maendeleo ya sehemu zote hizi
yalikua sawa, mwaka 2014 tujiulize,
c hangamoto kwetu ni vipi tutakua na
muungano utakaokua ni chachu ya maendeleo
ya haraka, mambo ya 74 ni tofauti na 2014′
5. ‘Tuwe makini sana, sote ni wa nchi moja,
tujiepushe na kikundi chochote kuona wao
wana haki zaidi, Watanzania wote sawa,
w ajumbe wa bunge maalum waangalie maslahi
ya nchi, muungano huu ni wa nchi 2 zilizokua
dola huru na kuungana kwa hiari’
6. ‘ Tupate katiba ambayo itaondoa migogoro,
kero iwe ni historia… hili swala lisiwepo tena,
t usiende kwenye maamuzi ya harahaharaka
tukasema serikali mbili au tatu bila kuangalia
athari zake, k atiba ya Znz inasema ni miongoni
mwa nchi mbili za muungano, ya Muungano
inasema Tz ni nchi moja, huo ni mgogoro’
7. ‘ Nadhani Warioba walivyopendekezwa
waliona hisia za Znz zilivyo, tunataka katiba
itakayotambua usawa wa nchi mbili, h akuwezi
kuwa na katiba ambayo itamridhisha kila mtu
lakini angalau wengi wao waridhike’
Hii ndio listi ya vilabu tajiri duniani – Real, Barca, Man U nani katisha????
Jarida la Forbes la marekani limeitaja klabu ya
Real Madrid kuwa na thamani ya €3.3 billion,
huku klabu ya Manchester United ikishika
nafasi ya pili ikiwa na thamani ya €3.16 billion.
Kumi 10 bora ya vilabu tajiri duniani
imetawaliwa na vilabu kutoka Premier League,
huku vilabu tajiri vya Ufaransa PSG
na AS Monaco vikiwa havitajwa kwenye listi
hiyo.
FORBES’ TOP 10 RICHEST CLUBS:
1) Real Madrid: €3.3 billion
2) Manchester United: €3.16 billion
3) FC Barcelona: €2.6 billion
4) Arsenal: €1.32 billion
5) FC Bayern Munich: €1.3 billion
6) AC Milan: €940 million
7) Chelsea FC: €900 million
8) Juventus: €690 million
9) Manchester City: €680 million
10) Liverpool FC: €650 million
MTU MMOJA AKAMATWA AKILA MAITI YA MTOTO HUKO PAKISTANI..
Ni visa mbavyo wengi tulivisikia katika hadithi
za kale, watu kuliwa na majitu, lakini katika
siku za karibuni tumeshuhudia watu wakila
viungo vya wenzao Jamhuri ya Afrika ya Kati
katika jazba ya kulipiza kisasi dhidi ya watu
waliowadhulumu katika uongozi uliong'olewa
mamlakani wa Seleka .
Nchini Pakistan Polisi wamewakamata wanaume
wawili kwa makosa ya kuiba maiti ya mtoto
kutoka kaburini na kisha kumla.
Wawili hao Arif Ali na kakake Mohammed Farman
Ali waliachiwa huru baada ya kuwa jela kwa
miaka miwili kwa kula nyama ya binadamu.
Hata hivyo wawili hao wameonekana kuwa na
tamaa kubwa ya mchuzi wa nyama ya
binadamu.Wakaazi hao wa kijiji cha Daryabn
Khan jimbo la Punjab walikamatwa mwaka 2011.
Polisi walisema kwamba walipata kiwiliwili cha
maiti ya msichana mdogo kikiwa bila miguu na
mikono.Wawili hao walikiri kwamba walipika
mchuzi wa nyama ya viungo hivyo na kuvila.
Walishtakiwa kwa makosa ya kuharibu kaburi
kwani nchini Pakistan hakuna sheria
inayozungumzia hatia ya mtu kumla mwenzie.
Punde baada ya kuachiwa Arif Ali aliambia BBC
kwamba anajutia makosa hayo na kwamba
hatarudia tena.
Hata hivyo punde si punde polisi wamesema
waliitwa na majirani wa jamaa huyo
wakilalamikia uvundo mkali kutoka kwa nyumba
yake.
Walipoingia chumbani humo Lo ! wakapata
kichwa cha mtoto.Kiwiliwili hakijulikani kililiwa au
kapotelea wapi. Arif Ali tena amekamatwa kwa
mara ya pili na polisi wanaendelea kumsaka
kakake.
Polisi wanaamini ndugu hawa walifukua maiti ya
mtoto ambaye kichwa kilipatikana ndani ya
makaazi yao.
Arif anamlaumu kakake Farman.Wawili hao
waliwahi kuoa na hata wakajaliwa watoto, hata
hivyo wake zao waliwatoroka kabla ya
kukamatwa kwao na kufungwa jela kwa kisa cha
awali.
JAMAL MALINZI AGOMA KUJIUZULU UENYEKITI WAKE
RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),
Jamal Malinzi amesema hatajiuzulu nafasi ya
Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa
Kagera (KRFA) pamoja na kuwa na majukumu ya
kitaifa.
Katika taarifa yake aliyoitoa mbele ya wajumbe
wa mkutano mkuu wa KRFA mkoani hapa juzi
Jumamosi, Malinzi alisema wakati anakuja
kuhudhuria mkutano huo alikuwa na wazo la
kujiuzulu.
Hata hivyo aliwaeleza wajumbe hao kuwa
ameachana na wazo la kujiuzulu nafasi ya
uenyekiti wa KRFA, kwa kuwa aliombwa na
wajumbe asichukue hatua hiyo.
Alisema baadhi ya wajumbe wa KRFA walitishia
kuachia nafasi zao endapo angejiuzulu nafasi
yake ndani ya chama hicho ili aendelee
kutumikia nafasi moja ya Rais wa TFF.
Pia alisema ameamua kuendelea ili kuzima
uvumi kutoka kwa wadau mbalimbali wa soka
waliodai kuwa aligombea nafasi ya uenyekiti wa
KRFA ili apate tiketi ya kugombea kiti cha urais
wa TFF.
Katika hotuba yake kwa wajumbe hao Malinzi
aliwataka kuhakikisha wanashirikiana na
halmashauri za wilaya ili kutenga maeneo ya
viwanja vya michezo na kusema Uwanja wa
Kaitaba utawekewa nyasi bandia baada ya
kupata ufadhili wa Shirikisho la Soka la
Kimataifa (Fifa).
SITTA"KUANZIA SASA TBC1 WAKIKATA MATANGAZO HATUWEZI KUKATISHA KUENDELEA NA BUNGE"
Jumamosi iliyopita matangazo ya Television ya
taifa yalikatika wakati ikiwa live kwenye bunge la
katiba ambapo Mh. Tundu Lissu alikua
akiwasilisha maoni ya wachache ambako
kulisababisha Mwenyekiti kuahirisha bunge hilo
mara moja baada ya kugundulika hawakuwa
wanaonekana live.
Kukatika huko kwa matangazo ambako badae
kulitangazwa kwamba ni kutokana na hali ya
hewa kulifanya TBC itupiwe lawama au
malalamiko yakiwemo kutoka kwa baadhi ya
viongozi na Wananchi huku baraza la habari
likisema ni kitendo cha aibu na watafatilia kujua
kama ni kweli hali ya hewa au hujuma.
Baada ya hayo yote na kauli zilizotolewa na
Wanasiasa mbalimbali baadae, Samwel Sitta
ambae ni Mwenyekiti wa bunge la katiba hapa
Dodoma ametoa taarifa rasmi akisema >>
‘kuanzia sasa matangazo ya live bungeni TBC1
yakikatika hatutawezi kukatisha kuendelea na
bunge’
‘Tunazingatia kwamba ipo Radio na Wananchi
wengi wa Tanzania wanasikiliza radio na mtu
mwenye TV hawezi kushindwa kununua radio
kwa hiyo hatuwezi kukatiza kila wakati, ikiwa
radio inaendelea kazi yetu humu ndani
itaendelea’ – Samwel Sitta
BREAKING NEWS:MAJAMBAZI WAVAMIA BENKI YA BARCLAYS TAWI LA KINONDONI
BREAKING NEWS: Watu wasiojulikana
wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wamevamia
benki ya Barclays tawi la Kinondoni na kupora
kiasi kikubwa cha fedha ambazo idadi yake
haijajulikana mara moja.
Tukio hilo limetokea muda wa saa nne , katika
tawi la benki hiyo iliyopo Kinondoni eneo la
Bakwata likihusisha watu watatu waliokuwa na
pikipiki mmoja wao akiwa na bastola.
Monday, 14 April 2014
KAULI YA MKUU WA MKOA WA ARUSHA JUU YA BOMU LILILOLIPUKA JANA USIKU NA IDADI YA MAJERUHI.
Usiku wa April 13 2014 kwenye baa iitwayo
‘Arusha night park’ iliyopo Mianzini Arusha
ambayo siku zote ni miongoni mwa sehemu
zinazokua na mkusanyiko wa watu wengi
kuanzia jioni, limerushwa bomu wakati watu
mbalimbali wakitazama mpira.
KITOMIXNEWS.. imepata nafasi ya kuongea na
mkuu wa mkoa wa Arusha ambae ni kiongozi
wa Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa
ambae amethibitisha kwamba ni watu 15
wamejeruhiwa kwenye mlipuko huo.
Anasema wote wamepelekwa hospitali ambapo
uchunguzi wa awali umeonyesha bomu hilo ni
la kutengenezwa kwa mkono na mpaka sasa
hajajulikana alietekeleza shambulio hilo.
Kwenye sentensi nyingine pia amesema hakuna
aliepoteza maisha kwenye shambulio hilo
ambalo uchunguzi wa awali umeshatoka, ila
baadae itatoka taarifa rasmi pale uchunguzi
kamili utakapokamilika.
Sunday, 13 April 2014
BREAKING NEWS .BOMU LALIPUKA TENA MKOANI ARUSHA.
Taarifa zilizo tufikia
hivi punde katika meza yetu ya habari hapa
KITOMIXNEWS zinasema kuwa watu kadhaa
wamejeruhiwa katika ajali ya bomu iliyotokea
hivi punde hapa mjini Arusha.
Ajali hiyo ni ya bomu imetokea katika baa ya
NIGHT PACK iliopo katika eneo la mianzini .
Tafadhali kwa habari zaidi endelea kuifwatilia
blogu hii ya KITOMIXNEWS......
REAL MADRID YAREJEA KILELENI LA LIGA
Madrid imehitimisha wiki nzuri kwa kurudi
kileleni mwa La Liga, baada ya usiku wa jana
kuitandika Almeria mabao 4-0, ikitoka kutinga
Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Ikicheza bila mwanasoka bora wa dunia,
Cristiano Ronaldo, Real ilipata mabao yake
kupitia kwa Angel Di Maria dakika ya 28, Gareth
Bale dakika ya 53, Isco dakika ya 56 na Morata
dakika ya 85.
Real sasa inatimiza pointi 79 za mechi 33 na
kupaa kileleni kwa wastani wa mabao kwa kuwa
na pointi sawa na Atletico Madrid, ikiizidi kwa
pointi moja Barcelona. Lakini Real wanaweza
kushuka hadi nafasi ya pili leo iwapo Atletico
Madrid itaifunga Getafe.
Katikati ya wiki, Real imeitoa Borussia Dortmund
katika Ligi ya Mabingwa Ulaya na kutinga Robo
Fainali, ambako itakutana na mabingwa watetezi,
Bayern Munich.
ARSENAL YATINGA FAINALI KOMBE LA FA
ARSENAL imetinga Nusu Fainali ya Kombe la FA
baada ya kuitoa Wigan kwa penalti 4-2 kufuatia
sare ya 1-1 ndani ya dakika 120 Uwanja wa
Wembley usiku huu.Baada ya kuitoa timu hiyo ya
Ligi Daraja la Kwanza England,maarufu kama
Championship, Arsenal sasa itakutana ama na
Hull City au Sheffield United Mei 17 katika fainali
Uwanja huo huo wa Wembley.
Ikiwa haijashinda taji lolote tangu waliposhinda
Kombe la FA mwaka 2005, Arsenal ilionekana
kupania kufanya vizuri leo, ingawa iliuanza
mchezo vibaya.
Wigan ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya
63 kupitia kwa Jordi Gomez aliyefunga kwa
penalty baada ya beki wa Arsenal, Per
Mertesacker kumuangusha kwenye eneo la hatari
Callum McManaman.
Hata hivyo, beki huyo Mjerumani ndiye aliyeifufua
Gunners katika mchezo wa leo baada ya kufunga
bao la kusawazisha dakika ya 82 na mchezo
ukahamia kwenye muda wa nyongeza.
Penalti mbili za mwanzo za Wigan ziliokolewa na
kipa Lukasz Fabianski, kabla ya kiungo wa
Arsenal, Santi Cazorla kufunga penalti ua ushindi
na kuipeleka timu hiyo fainali.
BARCELONA YAPIGWA NA KITIMU HICHO HADI AIBU
KLABU ya Barcelona imetimisha wiki ya
machungu baada ya kufungwa bao 1-0 na
Granada katika La Liga na kujiweka katika
mazingira magumu ya kutetea ubingwa, siku
chache baada ya kutolewa katika Ligi ya
Mabingwa Ulaya.
Bao la mapema la Yacine Brahimi lilitosha
kuwalizaa tena mabingwa wa zamani waq Ulaya
na sifa zimuendee kipa Orestis Karnezis,
aliyezuia michomo mingi akiichezea kwa mara
ya pili klabu hiyo, akiwatoa kapa Lionel Messi na
wenzake.
Barcelona inabaki na pointi zake 78 baada ya
mechi 33 katika nafasi ya pili, nyuma ya vinara
Atletico Madrid na wababe wao waliowatoa
Ulaya, wenye pointi 79 za mechi 32, wakati Real
Madrid ina pointi 76 za mechi 32 pia.
Friday, 11 April 2014
KUHUSU HABARI ZA MSANII SHETTA KUPATA AJALI YA GARI
Msanii Shetta wa bongofleva amepata ajali ya
gari maeneo ya Minjingu akielekea Babati kwa
ajili ya kufanya show ambayo maamuzi ya
kuifanya yalikuja dakika za mwisho.
Wakiwahi show kwa kutumia usafiri wa gari aina
ya Noah, walipata hiyo ajali jioni ya April 11
2014 baada ya gari kupinduka wakati dereva
akiwa kwenye jitihada za kumkwepa Punda.
Kwenye gari hilo, Shetta alikua na Msaidizi wake
pamoja na Waandaaji wa show ambapo hakuna
aliepoteza maisha isipokua majeraha
madogomadogo huku yeye mwenyewe akiumia
kichwani na mguuni.
Shetta alipelekwa hospitali lakini baadae
aliruhusiwa kuondoka na kuendelea na safari
japo haijajulikana kama aliweza kufanya hiyo
show baada ya kugundua kwamba alikua
ameumia kidogo.
SIRI NZITO ZA ALIKIBA ZAFICHUKA!!! SOMA HAPA
Wasanii wengi wa fani mbali mbali kuanzia
filamu hadi bongo fleva, wamekuwa wakipoteza
mashabiki wao wengi kutokana na ile hali tu ya
jinsi anavyochukulia umaarufu wake, kama
anatumia umaarufu wake vizuri basi hutokea
kupendwa sana na watu hata wale ambao siyo
mashabiki wake, watampenda tu kama mtu
wakawaida.Kismati hiki cha kupendwa sana na
watu wa rika mbalimbali anacho naye msanii
mkongwe sana Ali Kiba.
Ukimuongelea Msanii kama Ali Kiba, watu wengi
wanatamani wasanii wote wawe kama yeye,ni
mmoja kati ya wasanii wachache sana maarufu
ambao hawana ulimbukeni wa mali au umaarufu
wao, cause wengi wao pale wapatapo umaarufu
kidogo tu, huanza kudharau watu wake wa
karibu, haswa wakipata mali kidogo basi huishia
kuonyesha watu magari na
nyumba,hata kama haiwahusu, ilimradi tu basi
nao waonekane kama wasanii wa nje wenye mali
zao, ila kwa Ali kiba imekuwa ni tofauti sana,na
hiki ndicho kinachofanya AliKiba aweze
kupendwa zaidi na kila mtu.
Kupitia mtandao wa instagram Ali kiba aliweza
kuweka wazi mtazamo wake wa mafanikio:
“Kuishi maisha halisi yenye furaha na maana
kwako ni kitu cha thamani sana. Unayo kila
sababu ya kufuata njia yako ya maisha yenye
misingi mizuri ya kukujenga katika kila nyanja ya
maisha yako. Kwa kuwa kila mtu ana maono
yake binafsi kuhusu maisha ni vigumu kufafanua
maana halisi ya maisha. Naamini nawe pia una
falsafa yako ya kutafsiri nini maana ya maisha
mazuri kwako,”
AUNT EZEKIEL AFUKUZWA NYUMBANI KWA WEMA...KISA KIZIMA NA PICHA HIZI HAPA
MAPACHA WALIOUNGANA WAABUDIWA KAMA MIUNGU HUKO INDIA...CHEKI PICHA HAPA
Conjoined twins Shivanath and Shivram Sahu caused quite a stir when they were born in India, with some people in their village worshipping them as divine incarnations. And while one doctor has said that it would be possible to separate them, the 12-year-old boys, who were born joined at the waist, are determined to remain together.
MWANAMKE KAMA UNAPATA MAUMIVU WAKATI WA SEX NA MUMEO BAADA YA ROUND YA KWANZA AMA YA PILI FANYA HIVI.
1]-Kama hustahimili mzunguuko wa
tatu ambao labda nimrefu lakini
yeye haridhiki mpaka apige bao la
tatu basi msaidie kwa kumpa mikono
au mdomo na utakapohisi kuwa
anakaribia jirushe au jigeuze ili
akuingilie ukeni wakati bado uko
"tayari" hali itakayokufanya uepuke
maumivu kwani hatokupeleka
mwendo mreeeefu nakusababisha
maumivu
2] mkao/mtindo mnaotumia kufanya
mapenzi, kumbuka kuna mikao/
mitindo mingine husababisha
maumivu kwa mwanamke lakini
utamu kwa mwanaume, hivyo
unapaswa kutambua mikao gani
inawafaa wote wawili au kubadili
kila baada ya muda fulani kuliko
kushupalia mkao.mtindo mmoja
mwanzo mpaka mwisho.....hasa
kama mkao huo ndio
unakusababishia Discomfort.
3] mpenzi wako anakwenda mwendo
mrefu zaidi hali inayoweza
kusababisha mafuta ya Condom
kukauka, ute wako kidogo kukauka
na uke kuwa mkavu bila yeye
kujua....kwa kawaida ukitumia
Condom kwa zaidi ya dakika 15 au
pale unapohisi ukavu unapaswa
kubadilisha na kuvaa mpya.Unajua
baadhi ya wanaume wanaongeza
"mwendo" kutokana na mzunguuko,
mfano ikiwa mzunguuko wa kwanza
ulimalizika haraka labda ndani ya
Dk 10, mzunguuko wa pili unaweza
kumchukua Dk30, Mzunguuko wa
tatu ukaenda Dk45 mpaka saa na
kuendelea.
4] mnapofikia mzunguko wa tatu,
vilevile inawezekana huwa hauna
ute wa kutosha (kwa baadhi ya
wanawake mzunguuko wa 3 huitaji
kilainisho cha ziada kama mate au
Kay Jel) hali inayoweza
kukusababishia "sore" ukeni na hivyo
kuhisi maumivu pale unapoingiliwa.